Monday, March 14, 2016

AIRTEL FURSA YAINGIA DODOMA YATOA MSAADA WA SHS MILIONI 9

Afisa uhusiano na matukio wa Airtel, Dangio Kaniki (katikati), akijaribisha moja ya mashine mashine walizomkabidhi kijana Fikiri Chinji (kushoto), anayejishughulisha na ufundi seremala, kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’, katika hafla fupi iliyofanyika kwenye karakana yake iliyojengwa na Airtel katika Mtaa wa Ng’ong’ona manispaa Dodoma mwishoni mwa wiki hii. Anayeshuhudia (kulia) ni Meneja mauzo manispaa ya Dododma Hendrick Bruno.
Kijana Fikiri Chinji anayejishughulisha na ufundi seremala, akionyesha jinsi mashine yake mpya aliyokabidhiwa na Airtel Tanzania, kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’, inavyofanyakazi katika hafla fupi iliyofanyika kwenye karakana yake iliyojengwa na Airtel katika Mtaa wa Ng’ong’o na manispaa Dodoma mwishoni mwa wiki hii. Anayeshuhudia ni Meneja masoko manispaa ya Dodoma Saidimu Ngalesoni (kulia) akifuatiwa na Meneja mauzo manispaa ya Dodoma, Hendrick Bruno (wa pili kulia)
Afisa uhusiano na matukio wa Airtel, Dangio Kaniki (wa nne kulia), akimkabidhi kijana Fikiri Chinji (wa tano kushoto), anayejishughulisha na ufundi seremala, msaada wa vifaa mbali mbali vya ufundi na kujengewa karakana mpya kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’, katika hafla fupi iliyofanyika kwenye karakana yake iliyojengwa na Airtel katika Mtaa wa Ng’ong’ona manispaa Dodoma mwishoni mwa wiki hii. Wanaoshuhudia ni wanakijiji wa Ng’ong’ona na wafanyakazi wa Airtel waliofika kushuhudia tukio hilo.
Wanakijiji wa Mtaa wa Ng’ong’ona manispaa Dodoma wakiangalia banda alilokabidhiwa Kijana Fikiri Chinji (hayupo pichani) anayejishughulisha na ufundi seremala, pamoja na msaada wa vifaa mbali mbali vya ufundi kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’, mwishoni mwa wiki hii. 

No comments: