Tuesday, March 08, 2016

MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM, WAKUU WA WILAYA YA ILALA NA TEMEKE WATEMBELEA SHULE ZA MSINGI.

 Bodi ya Wakurugenzi wa Chama cha wamiliki wa Maroli Tanzania(TATOA) na Menejimenti leo iliungana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na Wakuu wa Wilaya wa Ilala na Temeke kutembelea shule za Msingi za Majimatitu, Mbande na kisongola ili kujionea hali halisi ya shule hizo na kujua changamoto mbalimbali wanazopitia.

 Hii ni katika kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika kuhakikisha kuwa watoto wote wanapewa elimu ya msingi bure. Wanachama wataendelea kupatiwa utaratibu wa namna ya kushiriki kuchangia juhudi hizi.


Bodi ya Wakurugenzi wa Chama cha wamiliki wa Maroli Tanzania(TATOA) na Menejimenti leo iliungana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick na Wakuu wa Wilaya wa Ilala, Raimond Mushi na Mkuu wa Wilaya ya Temeke walipotembelea shule za Msingi za Majimatitu, Mbande na kisongola ili kujionea hali halisi ya shule hizo na kujua changamoto mbalimbali wanazopitia.

No comments:

TUZINGATIE UTU, SHERIA NA HAKI KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YA ULINZI WA RASILIMALI ZA TAIFA- DKT KIJAJI

  Na. Joyce Ndunguru, Morogoro. Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Dkt Ashatu Kijaji (Mb) amewataka watumishi wa Mamlaka ya Usimamizi wa W...