Sunday, March 13, 2016

Rais Magufuli awathibitisha watendaji wakuu wa taasisi mbili za Serikali



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewathibitisha watendaji wakuu wa taasisi mbili za serikali.

Waliothibitishwa ni Bw. Alphayo Kidata, aliyekuwa Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ambaye anakuwa Kamishna Mkuu wa TRA, na Bw. Valentino Mlowola aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), ambaye anakuwa Mkurugenzi Mkuu wa (TAKUKURU).

Watendaji hawa wamethibitishwa kuanzia leo tarehe 13 Machi, 2016

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mawasiliano, IKULU.
Dar es salaam
13 Machi, 2016

No comments:

TUZINGATIE UTU, SHERIA NA HAKI KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YA ULINZI WA RASILIMALI ZA TAIFA- DKT KIJAJI

  Na. Joyce Ndunguru, Morogoro. Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Dkt Ashatu Kijaji (Mb) amewataka watumishi wa Mamlaka ya Usimamizi wa W...