Saturday, March 26, 2016

MWANASHERIA MKUU ZANZIBAR AAPISHWA RASMI LEO


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Said Hassan Said kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar katika hafla iliyofanyika leo Ikulu Mjini Zanzibar.
Pichani Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Said Hassan Said.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.ALi Mohamed Shein akiwa katika picha na Said Hassan Said Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar na familia yake baada ya kumuapisha rasmi leo katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar.
Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Said Hassan Said akipitia hati ya kiapo kabla ya kuapishwa leo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.ALi Mohamed Shein hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano Ikulu Mjini Unguja.
Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar Nd,Ibrahim na Mzee na Mrajis wa Mahkama Kuu Zanzibar George Kazi ni miongoni mwa Viongozi waliohudhuria katika hafla ya kuapishwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Said Hassan Said leo Ikulu Mjini Unguja.
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe,Abdalla Mwinyi Khamis na Mstahiki Meya wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib ni miongoni mwa Viongozi waliohudhuria katika hafla ya kuapishwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Said Hassan Said leo Ikulu Mjini Unguja.
Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Said Hassan Said akiwa katika ukumbi wa mikutamo Ikulu Mjini Unguja na Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar, Mshibe Ali Bakari kabla ya kuapishwa leo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.ALi Mohamed Shein.
Viongozi mbali mbali na watendaji waliohudhuria katika hafla ya kuapishwa Said Hassan Said kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar katika ukumbi wa mikutano Ikulu Mjini Zanzibar leo asubuhi.

No comments: