Sunday, March 06, 2016

RAIS MAGUFULI AMTEUA BALOZI JOHN WILLIAM KIJAZI KUWA KATIBU MKUU KIONGOZI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Balozi Mhandisi John Kijazi kuwa Katibu Mkuu Kiongozi.
Kabla ya Uteuzi huo, Mhandisi Kijazi alikuwa Balozi wa Tanzania nchini India.
Kufuatia uteuzi huo, aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue atapangiwa kazi nyingine.
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
06 Machi, 2016.

No comments: