Thursday, March 17, 2016

KAMATI YA BUNGE YA MAMBO YA NJE YAKUTANA NA UONGOZI WA WIZARA YA MAMBO YA NJE

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Mhe. Balozi Adad Rajab akimkaribisha Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Susan Kolimba (hayupo pichani) kuwasilisha taarifa ya Wizara kuhusu Sera, Muundo na Majukumu kwa Wajumbe wa Kamati hiyo. Kikao hicho ambacho kiliwahusisha pia Wakurugenzi kutoka Wizarani kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 15 Machi, 2016.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Susan Kolimba akiwasilisha mada kuhusu Sera, Muundo na Majukumu ya Wizara kwa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (hawapo pichani)
Sehemu ya Wabunge wakimsikiliza Naibu Waziri alipowasilisha taarifa ya Wizara.
Mkurugenzi wa Chuo cha Diplomasia kilichopo Kurasini Jijini Dar es Salaam, Balozi Mohammed Maundi akiwasilisha taarifa ya utendaji ya Chuo hicho ambacho ni moja ya Taasisi za  Wizara
Wabunge wakifuatilia uwasilishwaji wa taarifa za Wizara
Katibu Mtendaji wa Mpango wa Nchi za Afrika kujitathmini kiutawala Bora (APRM) kwa upande wa Tanzania, Bibi Rehema Twalib akiwasilisha taarifa kuhusu taasisi hiyo ambayo ipo chini ya Wizara ya Mambo ya Nje
Sehemu nyingine ya Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama wakiwa kikaoni
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Bw. Elishilia Kaaya naye akiwasilisha taarifa ya kituo hicho kwa Kamati ya Bunge.
Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Wizarani wakifuatilia uwasilishwaji wa taarifa
Wakurugenzi
Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Wizarani wakati wa kikao
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi akitolea ufafanuzi baadhi ya hoja wakati wa kikao na Kamati ya Bunge
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati wakifuatilia.
Sehemu nyingine ya Wakurugenzi wa Wizara
Mkutano ukiendelea
Mhe. Dkt. Kolimba akizungumza na Waandishi wa Habari

No comments: