Sunday, March 20, 2016

DKT SHEIN AONGOZA WAZANZIBARI KUPIGA KURA UCHAGUZI WA MARUDIO LEO


 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  ambae ni mgombea wa Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Dk.Ali Mohamed Shein akipiga kura katika uchaguzi wa marudio  kituo namba 1cha kupiga kura namba 1 Skuli ya   msingi Bungi Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja leo,Wananchi wa Zanzibar leo wanapiga kura katika uchanguzi wa marudio baada ya kufutwa kwa uchanguzi uliofanyika October 25,2025 kutokana na kasoro zilizojitokeza.
 Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Ally Iddi akiwa katika maandalizi ya kupiga kura katika uchaguzi wa marudio kituo cha Skuli ya Kitope, Wilaya ya Kaskazini B , Mkoa wa Kaskazini. 
  Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Ally Iddi akipiga kura katika uchaguzi wa marudio katika kituo cha Skuli ya Kitope, Wilaya ya Kaskazini B , Mkoa wa Kaskazini. 
  Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Ally Iddi akizungumza na baadhi ya Waandishi wa Habari mara baada ya kupiga kura katika uchaguzi wa marudio kwenye kituo cha Skuli ya Kitope, Wilaya ya Kaskazini B , Mkoa wa Kaskazini. 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh.January Makamba akizungumza na Waandishi wa habari akielezea hali halisi ya mwenendo wa upigaji kura katika uchaguzi wa marudio  kituo namba 1cha kupiga kura namba 1 Skuli ya   msingi Bungi Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja leo.
 Mkazi wa chake chake akizungumza.na  wanahabari ( hawapo pichani) mara baada ya kutoka kupiga kura
Baadhi ya Wakazi wa Madungu wakiangalia majina yao kwenye kituo cha kupigia kura
kituo cha kupigia kura cha skuli ya Madungu chake chake Pemba.
Baadhi ya wananchi wakihakiki majina yao kabla ya kuingia kupiga kura katika kituo cha skuli ya Raha Leo.

No comments: