Wednesday, March 16, 2016

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA NA SERIKALI ZA MITAA YATEMBELEA TAKUKURU NA SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA

1Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akitoa ufafanuzi kuhusu masuala yaliyoulizwa wakati wa kikao.
2Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Bw. Valentino Mlowola akitoa maelezo kuhusu taasisi anayoiongoza kwa wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa.
3Mwenyekiti wa Kamati ya Kuduma ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Mhe. Jason Rweikiza (Mb) akitambulisha kamati anayoiongoza.
4Mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Mhe. Ruth Mollel (Mb) akitoa mchango wake katika kikao.
5Sehemu ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa (mkono wa kushoto) wakisalimiana na wafanyakazi wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kabla ya kikao.
6Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Xvier Daudi akiwasilisha mada kuhusu taasisi anayoiongoza kwa wajumbe wa kamati ya Bunge, hawapo pichani.
7Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Utumishi Dkt. Laurean Ndumbaro, kushoto, akitoa ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali ya kiutumishi wakati wa kikao na kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kilichofanyika Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.
8Waziri wa Nchi, Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angellah Kairuki (Mb) kulia, akifafanua jambo wakati wa kikao na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kilichofanyika Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.

No comments: