Friday, October 09, 2015

UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI JENGO LA ABIRIA TERMINAL II ZANZIBAR

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na mwakilishi wa Balozi wa China nchini Tanzania ambaye anafanyia kazi Zanzibar  Chein Li wakati alipowasili katika uwekaji wa jiwe la Msingi ujenzi wa jengo jipya la Abiria Terminal II katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar leo,jengo hilo linajengwa na kampuni kutoka China
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi mbali mbali wa Serikali wakati alipowasili katika uwekaji wa jiwe la Msingi ujenzi wa jengo jipya la Abiria Terminal II katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar leo,ujenzi  wa jengo hilo unajengwa na Kampuni kutoka China
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akifungua pazia kama ishara ya uwekaji wa Jiwe la msingi ujenzi wa jengo jipya la Abiria Terminal II linalojengwa na kampuni kutoka China katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar leo,(katikati) Naibu waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Issa Haji Ussi (GAVU)
 Misimamizi wa  Mradi  kwa upande wa Serikali ya Mapinduzi Yasser De Costa katika Ujenzi wa jengo jipya la Abiria Terminal II linalojengwa na kampnuni ya Kichina katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar akitoa maelezo ya maendeleo ya ujenzi huo alipotembelea baada ya kuweka jiwe la msingi leo katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akiwa nje ya jengo jipya la Abiria Terminal II ilnalojengwa na kampuni ya kichina katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar  na kupatiwa maelezo ya ujenzi na Msimamisi wa Mradi  kwa upande wa Serikali ya Mapinduzi  Yasser De Costa,baada ya kuweka Jiwe la msingi ujenzi huo leo.


No comments: