Thursday, October 22, 2015

AIRTEL SMARTIFONIKA YALETA SIMU MPYA SOKONI NAFUU KULIKO ZOTE

 Afisa Uhusiano na Matukio wa Airtel Bi Dangio Kaniki akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati Airtel ilipozindua  smartifoni mpya ijulikanayo kama Magnus Bravo Z10zitakazopatikata katika maduka yote ya Airtel zikiwa zimeunganishwa na ofa ya Smartifonika  kutoa  muda wa maongezi wa dakika 150, 150MB na SMS 150 kwa kipindi cha miezi sita. Kulia ni bi Anethy Muga meneja masoko wa Airtel. Hafla ya uzinduzi imefanyika jana katika makao makuu ya Airtel Dar es salaam
 Meneja Masoko wa Airtel Bi Anethy Muga akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati Airtel ilipozindua  smartifoni mpya ijulikanayo kama Magnus Bravo Z10 zitakazopatikata katika maduka yote ya Airtel zikiwa zimeunganishwa na ofa ya Smartifonika  kutoa  muda wa maongezi wa dakika 150, 150MB na SMS 150 kwa kipindi cha miezi sita. Kushoto ni Afisa Matukio wa Airtel Bi, Dangio Kaniki wakati wa Hafla ya uzinduzi iliyoyika jana katika makao makuu ya Airtel Dar es salaam.
 Afisa Uhusiano na Matukio wa Airtel Bi Dangio Kaniki (kushoto) akiwa na  Meneja masoko wa Airtel Anethy Muga (kulia) wakionyesha simu mpya zilizoingizwa sokoni zikiwa na ofa ya Airtel smartifonika aina ya Mgnum Bravo Z10 wakati wa hafla ya uzinduzi iliyofanyika makao makuu ya Airtel leo
Afisa Uhusiano na Matukio wa Airtel Bi Dangio Kaniki akijaribu kupiga picha kwa kutumia kamera ya mbele ya simu mpya aina ya Magnus Bravo Z10 inayopatikana katika maduka ya Airtel kuanzia sasa ikiwa na ofa ya Smartifonika, uzindunzi wa kuingiza sokoni simu hii yenye uwezo wa kutumia  laini mbili umefanyika jana katika makao makuu ya Airtel.

  AIRTEL  Tanzania leo imezindua smartifoni mpya na yenye ubora zaidi ijulikanayo kama Magnus Bravo Z10 ambapo zinapatikata sasa hivi  kwenye maduka yote ya Airtel nchini zikiwa zimeunganishwa na ofa ya Smartifonika  inayompatia mteja muda wa maongezi wa dakika 150, 150MB na SMS 150 kwa kipindi cha miezi sita.

Akiongea na waandishi wa habari Meneja masoko wa Airtel Tanzania Aneth Muga amesema “Airtel tumekuletea Simu mpya ya Magnus Bravo Z10 ili kukuwezesha mteja wetu kuendelea kufurahia huduma zote za Airtel na zile huduma zote za kisasa za smartifoni ukiwa mahali popote
 “Magnus Bravo Z10 toka Airtel inatumia laini mbili, ina radio, kioo (screen) kubwa ili kukupa raha zaidi kuona vyema unapokuwa unaitumia, pia imewekewa kamera zenye uwezo mkubwa mbele na nyuma za 5mp ili kukupa taswira au picha nzuri utakazopiga karibu au mbali ukiwa na ndugu, jamaa na marafiki” alielezea Bi Muga
“Vilevile ili  uweze kufurahia huduma zote za mitandao, Airtel tumehakikisha tayari simu hii inamitandao yote ya kijamii kama facebook, Instagram, twitter na mingine mengi” . Alisema Bi Muga
Simu hii inapatikana sasa katika maduka yote ya Airtel nchini kwa gharama nafuu kuliko zote ya sh. 75,000  tu.

No comments: