Sunday, October 18, 2015

MGOMBEA UWAKILISHI JIMBO LA TUNGUU, MBUNGE NA MADIWANI WAENDA KIJIJI KWAO SIMAI MUHAMMED UZI MTONGANI KUOMBA KURA.

1

Mwenyekiti wa CCM wadi ya Tunguu Omar Azan Jecha akiwasalimi wananchi wa wadi ya Bungi waliofika kwenye Mkutano wa kuwanadi wagombea wa Chama cha Mapinduzi CCM katika Mkutano uliofanyika kiwanja cha mpira cha Uzi Mtongani Mkoa wa Kusini Unguja.
2
Mgombea uwakilishi Jimbo jipya la Tunguu Simai Muhammed Said (alievaa miwani waliokaa chini) akiwa na wananchi wa kijijini kwao Uzi wakimsikiliza Mwenyekiti wa CCM wadi ya Tunguu Omar Azan Jecha (hayupo pichani) alipokuwa akiwatambulisha wageni waliofika kwenye Mkutano huo.
4
Mgeni rasmin Waziri wa Ardhi, Makazi na Nishati Zanzibar anaemaliza muda wake Mhe. Ramadhan Shaaban akimtambulisha mgombea Ubunge Jimbo jipya la Tunguu Khalifa Salum Suleiman wakati wa Mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika uwanja wa mpira wa Uzi Mtongani jana Oct 17.
5
Mgombea uwakilishi Jimbo jipya la Tunguu Simai Muhammed Said akiwasalimia wananchi waliofika kwenye Mkutano uliofanyika kijijini kwao Uzi.
7
6
Mgeni rasmin kwenye Mkutano huo Mhe. Ramadhan Shaaban akinadi mgombea uwakilishi Jimbo jipya la Tunguu kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi CCM Simai Muhammed Said wakati wa Mkutano wa wadi ya Bungi uliofanyika Uzi Mtongani Mkoa Kusini Unguja.
PICHA NA MAKAME MSHENGA -MAELEZO ZANZIBAR

No comments: