Friday, October 23, 2015

RAIS KIKWETE AAGANA NA WATUMISHI WA UMMA

7

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwahutubia viongozi na wawakilishi wa Watumishi wa Umma katika ukumbi wa Mlimani City wakati wa Sherehe ya Watumishi wa Umma Kumuaga Rais jana.
(Picha na Freddy Maro).
1
Katibu Mkuu Kiongozi na Mkuu wa Utumishi wa Umma Balozi Ombeni Sefue akimkabidhi Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete orodha ya zawadi mbalimbali kutoka katika taasisi za umma wakati wa sherehe ya watumishi wa umma kumuaga Rais iliyofanyika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam jana.
3
Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Dkt.Edward Hosea kwa niaba ya watumishi wa Umma akimkabidhi Tuzo Maalum Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete kwa kutambua mchango wake katika kuboresha Utumishi wa Umma nchini wakati wa  sherehe ya Watumishi wa Umma Kumuaga Rais iliyofanyika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam jana usiku.
5
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania Bwana Awadh Masawe akimkabidhi Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete mfano wa ufunguo wa trekta alilokabidhiwa na watumishi wa taasisi za umma jana wakati wa sherehe za kumauaga Rais katika ukumbi wa Mlimani City jana.
6
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete,Katibu Mkuu Kiongozi na Mkuu wa Utumishi wa Umma Balozi Ombeni Sefue,Jaji Mkuu Othman Chande,Mwanasheria Mkuu Mh.George Masaju pamoja Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Bwana Florence Turuka wakiwa katika picha ya pamoja na Makatibu wakuu wa Wizara Mbalimbali wakati wa Sherehe ya Watumishi wa Umma Kumuaga Rais iliyofanyika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam jana

No comments: