Wednesday, October 21, 2015

UMMOJA WA WANANCHI WA KIBADA WAFANYA MATENGENEZO GARI LA JESHI LA ZIMAMOTO



Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi iliyofanikisha upatikanaji wa Gari  la zimamoto, Mussa Bibose akitoa maelekezo kwa wananchi waliohudhuria shughuli ya kukabidhi gari hilo Kibada,Kigamboni  Jijini Dar es salaam. 

Mwenyekiti wa Umoja wa wananchi wa Kibada, Kigamboni Jijini Dar es salaam Bwana Lagano Mwampetu akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya gari moja ya zimamoto iliyopatikana kwa Juhudi za umoja huo na kukabidhi kwa  Kamishna wa Operation Jeshi La Zimamoto na uokoaji Tanzania CF, Rogatus Kipali.

Kamishna wa Operation Jeshi La Zimamoto na uokoaji Tanzania CF, Rogatus Kipali akiangumza na wananchi waliojitokeza wakati wa kukabidhi Gari hilo ambapo amewapongeza wananchi wa Kibada kwa juhudi kubwa za kuhakikisha kuwa wanaleta maendeleo katika maeneo yao.

Mwenyeikiti wa umoja wa wananchi wa Kibada, Kigamboni Jijini Dar es salaam Lugano Mwampeta akimpa maelekezo kamishna wa Operation jeshi la zimamoto na uaokoaji Tanzania CF, Rogatus Kipali wakati wa shughuli ya kumkabidhi gari moja la kuzima moto lililofanyiwa matengenezo kwa nguvu ya wananchi wa kibada kwa ajili ya kuwasaidia wakazi hao na majanga ya moto,makabidiano hayo yaliyofanyika Kigamboni Kibada Jijini Dar es salaam.

Gari la Jeshi la Polisi la zimamoto lilofanyiwa matengenezo na wananchi wa Kibada Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Jeshi la Polisi wakifanya zoezi la uzimaji moto mara baada ya kukabidhiwa gari hilo.

No comments: