Monday, October 19, 2015

MAHAFALI YA KWANZA YA SHULE YA SEKONDARI ADILI HIGH SCHOOL MOSHONO JIJINI ARUSHA

Mgeni Rasmi katika Mahafali ya kwanza ya Shule ya Sekondari Adili High School,Moshono Jijini Arusha,Profesa Raymond Mosha akiangalia kazi zilizoandaliwa na wanafunzi wa masomo ya Sayansi ikiwa ni sehemu ya mahafali ya kidato cha Nne.

Wazazi wa wanafunzi wanaotarajia kuhitimu Kidato cha Nne wakifatilia kazi za ubunifu zilizoandaliwa kwaajili ya kuonesha uwezo wao katika masomo ya Sayansi kwenye  Mahafali ya kwanza ya Shule ya Sekondari Adili High School.

Wahitimu wakiwa na nyuso za tafakari kwenye mahafali ya kwanza ya Shule Adili High School iliyopo Moshono,Jijini Arusha. 

Wanafunzi hao wakionesha igizo linalopiga vita ukeketaji kutokana na madhara yake kwa wanawake jambo linaloweza kusababisha ulemavu wa kudumu na vifo.

Profesa Raymond Mosha akizungumza kwenye mahafali hayo,amesisitiza maadili kama msingi mkuu wa mafanikio katika masomo na utendaji kazi,kushoto ni Mkuu wa Shule hiyo,Mwalimu Andrew Shayo na Mwenyekiti wa bodi ya shule,Wakili Modest Akida.
Baadhi ya wafanyakazi wa Shule ya Sekondari Adili High School .

Mwanafunzi Nolam Mike akipokea cheti cha kuhitimu masomo yake kutoka kwa mgeni rasmi.

Wafanyakazi wakiburudika mbele ya wazazi na mgeni rasmi wakifurahia wahitimu wa kwanza wa kidato cha Nne.

No comments: