Wednesday, October 28, 2015

RAIS KIKWETE APOKEA HATI ZA UTAMBULISHO KUTOKA KWA MABALOZI WANNE

JA1
Balozi mpya wa Misri hapa nchini Mhe.Yasser Ahmed Al Eldin Elshawaf wakiwalisha hati zake za utambulisho kwa Rais Kikwete ikulu jijini Dar Es Salam leo.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo amepokea hati za utambulisho kutoka kwa mabalozi wanne wanaziwakilisha nchi zao hapa Tanzania.Mabalozi waliowasilisha hati zao kwa Rais Kikwete ikulu asubuhi ya leo ni pamoja Mhe.Yasser Ahmed Al Eldin Elshawaf Balozi mpya wa Misri hapa nchini, Mhe.Yahel Vilan Balozi mpya wa Israel nchini Tanzania, Mhe.Bayani Mangibin balozi mpya wa Ufilipino nchini na Mhe. Tan Puay Hiang Balozi mpya wa Singapore nchini Tanzania.
Pichani Mabalozi hao wakiwasilisha hati zao za utambulisho.
JA2
-Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipokea hati za utambusho kutoka kwa Mhe.Yahel Vilan Balozi mpya wa Israel hapa nchini,
JA3
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipokea hati za utambulisho kutoka kwa mhe.Bayani Mangibin Balozi mpya wa Ufilipino nchini Tanzania.
JA4
-Balozi mpya wa Singapore nchini Tanzania Mhe.Tan Puay Hiang akiwasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es salaam leo(picha na Freddy Maro) 

No comments: