Tuesday, September 01, 2015

WAKAZI WA JIJI LA DAR ES SALAAM WAENDELEA KUNUFAIKA NA HUDUMA ZA MAWASILIANO


  Ofisa Mkuu wa Idara ya Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania, Keith Tukei (katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa duka jipya la Vodacom Tanzania lililopo katika maduka ya Shoppers plaza Mbezi Beach jijini Dar es Salaam.Wengine katika picha kushoto ni mteja wa kwanza kufika kupata huduma katika duka hilo Bw.Argylle Tsvakai na Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa kampuni hiyo, Rosalynn Mworia.
 Mteja wa kwanza kufika katika duka jipya la Vodacom Tanzania Bw.Argylle Tsvakai (kulia) akiangalia moja ya simu zinazouzwa kwa bei nafuu katika duka hilo lililopo katika maduka ya Shoppers Plaza Mbezi Beach jijini Dar es Salaam baada ya kuzinduliwa rasmi na Afisa Mkuu wa Idara ya Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania, Keith Tukei (kushoto). Katikati ni Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa kampuni hiyo, Rosalynn Mworia.
Ofisa Mkuu wa Idara ya Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania, Keith Tukei (kushoto) akimmiminia mvinyo kwenye glasi Bw.Argylle Tsvakai ambaye alikuwa ni mteja wa kwanza kufika kupata huduma katika duka jipya la kampuni hiyo  lililopo katika maduka ya Shoppers Plaza Mbezi Beach jijini Dar es Salaam baada ya kuzinduliwa rasmi leo. Anayeshuhudia katikati ni Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa kampuni hiyo, Rosalynn Mworia. 
 Baadhi ya waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari nchini wakimfanyia mahojiano Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Rosalynn Mworia baada ya kuzinduliwa kwa duka jipya la kampuni hiyo lililopo katika maduka ya Shoppers Plaza Mbezi Beach jijini Dar es Salaam.
Picha ya pamoja ya baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania na wadau wao walioshiriki katika uzinduzi wa duka jipya la kampuni hiyo leo lililopo katika maduka ya Shoppers Plaza Mbezi Beach jijini Dar es Salaam.

No comments: