Bi. Vanessa Anyoti kutoka YWCA Tanzania (kushoto) akizungumza kuhusiana masuala ya kijinsia pamoja na maendeleo ambayo yanaweza kupunguza maabukuzi ya virusi vya UKIMWI. Kulia niMkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi naUtamaduni (UNESCO), Bi. Zulmira Rodrigues
MWENYEKITI WA MTANDAO WA KIMATAIFA WA VIONGOZI WA DINI WAISHIO NA VVU/UKIMWI NA WALIYOATHIRIWA NA UKIMWI (INERELA+) MCH. MPUMZILE MABIZELA AKIZUNGUMZA NA VIONGOZI WA NGAZI YA JUU WA DINI NA WAWAKIRISHI WA DINI KUTOKA NCHI 17 ZA MASHARIKI NA KUSINI MWA AFRIKAWAKATI WA MKUTANO ULIOANZA LEO JIJINI DAR.
MKURUGENZI MKAZI WA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA ELIMU, SAYANSI NAUTAMADUNI (UNESCO), BI. ZULMIRA RODRIGUES AKISOMA HOTUBA KWA VIONGOZI WA NGAZI YA JUU WA DINI NA WAWAKIRISHI WA DINI WALIOFIKA KWENYE MKUTANO ULIOFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM, TANZANIA KUJADILI NA KUWEKA MIKAKATI YA KUHARAKISHA KUMALIZAMA AMBUKIZI MAPYA YA VVU/UKIMWI
DK.WARREN NAMARA KUTOKA SHIRIKA LA (UNAIDS) AKIELEZEA NI KWA NJIA GANI VIONGOZI WA KIDINI WANAWEZA KUELIMISHA JAMII INAYOWAZUNGUKA JINSI YA KUPANBANA NA KUEPUKA MAAMBUKIZI MAPYA YA VIRUSI VYA UKIMWI.
MWENYEKITIWA TUME YA KUDHIBITI UKIMWI TANZANIA (TACAIDS) DK. FATMA MRISHO AKITOA WITO KWA MASHIRIKA MBALIMBALI KUJIKITA KATIKA UTOAJI WA ELIMU KUHUSU MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI HUKU WAKISHIRIKIANA NA VIONGOZI WA NGAZI YA JUU WA DINI.
……………………………………………….
Na Mwandishi Wetu
Viongozi wa ngazi ya juu wa dini na wawakilishi wa dini
kutoka nchi 17 za Mashariki na Kusini mwa Afrika wamekutana Dar es Salaam, Tanzania
kujadili na kuweka mikakati ya kuharakisha kumaliza maambukizi mapya ya VVU/Ukimwi
.
Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO)
kwa kushirikiana na mtandao wa kimataifa
waviongozi wa dini wanaoishi ua waliyoathiriwa na virusi vya Ukimwi (INERELA+) pamoja na Shirika
la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya Ukimwi na mtandao wa kimataifa wa viongozi wa dini wanaoishi
ua waliyoathiriwa na virusi vya ukimwi (INERELA+)
wameandaa mkutano wa siku tatu wa
kimataifa kujadili ushiriki wa taasisi na viongozi wa dini katika kukabiliana
na maambukizi mapya ya VVU/Ukimwi.
Mkutano huo ulioanza jana tarehe 02/09/2015 unafanyika
katika Hotel ya Kunduchi, Dar es Salaam, Tanzania na unaohudhuliwa na zaidi ya
viongozi 50 wangazi ya juu wa dini na wawakilishi wa mtandao wa INERELA+ kutoka
nchi 17 za Mashariki na Kusini mwa Afrika ikiwemo Tanzania.
Wengine wanaohudhuria mkutano huo ni wawakilishi wa makundi ya
vijana; wawakilishi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na wawakilishi wa taasisi za
serikali ikiwemo tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania na Unesco Tanzania.
Katika mkutano huo Mwenyekiti wa Mtandao wa kimataifa wa
viongozi wa dini waishio na VVU/Ukimwi na waliyoathiriwa na Ukimwi (INERELA+) Mch.
Mpumzile Mabizela ameeleza umuhimu wa kiongozi wa dini na namna kiongozi wa
dini anavyoweza kushiriki katika kutoa elimu kuhusu maambukizi ya Ukimwi, matumizi
sahihi ya dawa zakupunguza makali ya VVU, unyanyapaa na namna watu wanavyoweza
kujikinga na maambukizi kupitia semina mbalimbali zinazokuwa zikiendelea katika
misikiti na madhehebu mbalimbali.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa
la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bi. Zulmira Rodrigues amewataka
viongozi wa dini kujikita katika jamii kwa ajili ya kutoa elimu inayohusu
virusi vya Ukimwi hususani kwa vijana na jamii iliyopo vijijini.
Aliongeza kuwa kutokana na sababu za kiutamaduni na mila
wazazi wengi wanashindwa kuongea na watoto juu ya masuala ya jinsia, balehe na
mahusiano hii inachangia vijana wengi kukosa elimu sahihi juu ya miili yao
hususani afya ya uzazi na kujikuta wanapatamatatizo ikiwemo mimba za utotoni na
maambukizi ya VVU.
Akisistiza umuhimu wa viongozi wa dini katika mapambano
dhidi ya Ukimwi na mimba za utotoni, Bi Zulmira aliwataka viongozi hao
kushiriki kikamirifu katika kutoa elimu sahihi na kujiepusha na ushauri utakaowasaidia
waamini na vijana.
“Wakati dunia
inategemea mchango wenu katika kuhakikisha watu wanazingatia matumizi sahihi ya
dawa, baadhi yenu mmekuwa mkitoa elimu zinazochangia watu kuacha matumizi ya
dawa na hatimaye kuathiri kinga zao za mwili,”alisema Zulmira.
Aligusia suala la unyanyapaa na namna viongozi wa dini
wanavyoweza kusaidia kupunguza “msiwatenge na kuwanyanyapaa watu wanaoishi na
virusi vya Ukimwi kwani wanahitaji elimu zaidi ili waweze kuwa katika hali ya
kawaida nasi ya kiunyonge,”alisema.
Naye Mwenyekitiwa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS)
Dk. Fatma Mrisho alitoa wito kwa mashirika mbalimbali kusaidiana na viongozi wa
kidini katika kuhakikisha watu wana hamasikana kupima afya zao kila wakati na
kusambaza elimu inayohusu maambukizi ya virusi vya Ukimwi kwa maeneo mbalimbali
na pia aliwaasa vijana ambao bado ni wadogo kutokujiingiza katika ulimwengu wa
ndoa kwani vitendo hivyo vinachangia kwa kasi maambukizi mapya ya VVU.
Kwa upande wake Dk.Warren Namara kutoka Shirika la UNAIDS aliongeza kuwa viongozi wa dini ni viongozi waaminifu waadilifu na ni
waelimishaji.
Kulingana na huduma yao ya kukutana na waumini kila wiki
wana nafasi nzuri na pia ni rahisi sana kuweza kuwafikishia ujumbe na
kuwaamasisha wananchi katika maeneo yao kwa kutoa elimu ya virusi vya ukimwi.
dk warren alisisitiza haki ya kila mtu kupata elimu sahihi na kuwataka viongozi
wa dini kutowatenga watu hasa waliyo kwenye hatari zaidi ya kupata maambukizi
mfano watu wanaotumia madawa ya kulevya na watuwanaofanya biashara ya kuuza
miili yao.
Mshereheshaji wa mkutano huo Prof. Venant Nantulya akiwa katika hatua ya uendeshaji wa mkutano wa Viongozi wa ngazi ya juu wa dini katika kupambana na kuweka mikakati ya kuharakisha kumalizama ambukizi mapya ya VVU/UKIMWI.Picha na Geofrey Adroph
Mufti mkuu wa Zambia, Sheikh Assadullah Mwale akifungua kwa dua katika mkutano wa viongozi wa dini wa nchi za mashariki na kusini mwa Afrika uliofanyika leo jijini Dar.
Baadhi ya Viongozi wa ngazi ya juu wa dini na wawakirishi wa dini kutoka nchi 17 za Mashariki na Kusini mwa Afrika wakiwa kwenye mkutano huo utakaodumu kwa takribani siku tatu.
Picha ya Pamoja Kwa washiriki walio hudhuria mkutano huo.
No comments:
Post a Comment