Saturday, October 03, 2015

MAMA SAMIA AZURU KABURI LA BABA WA TAIFA MWALIMU NYERERE

Msafara wa Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan ukiwasili nyumbani kwa familia ya Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ambako alika kusalimia familia hiyo na kuzuru kaburi la Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, Octoba 2,2015 katika Kijiji cha Mwitongo, Butiama, akiwa kaika ziara ya kufanya mikutano ya kampeni katika mkoa wa Mara.
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akimsalimia mtoto wa sita wa Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Nyerere, Madaraka Nyerere, alipowasili nyumbani kwa familia ya Baba wa Taifa huyo, katika Kijiji cha Mwitongo, Bitiama mkoani Mara.
 Mama Samia akisalimia wanafamilia wa Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Nyerere
 Mama Samia akisalimia wanafamilia wa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere
 Chifu wa Ukoo wa Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Nyerere, Japhet Wanzagi, akimkaribisha na kutoa utambulisho kwa Mgombea Mweza wa Urais Mama Samia Suluhu Hassan,
 Aliyekuwa Muomba nia ya kugombea Ubunge jimbo la Nkenge, Asupta Mshama, akipozi kwenye baadhi ya miamba ya mawe iliyopo katibu na kaburi la Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Nyerere, katika Kijiji cha Mwsenge, Butiama mkoani Mara.
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akiwasha mshumaa baada ya kuweka shada la maua kwenye kaburi la Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Nyerere, Mwitongo, Butiama mkoani Mara.
Mama Samia akishiriki kuomba dua kwenye kaburi la Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Nyerere, kijiji cha Mwitongo, Butiama mkoani Mara.
Mama Samia akiondoka baada ya kuzuru kaburi la Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Nyerere. Butiama mkoani Mara.
PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

No comments: