Monday, October 05, 2015

MAMA SALMA KIKWETE KATIKA TAMASHA LA KUOMBEA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2015.

5
Mke wa Rais ,Mama Salma Kikwete akipokea Tuzo  Maalum kwa niaba ya Rais Dkt. Jakaya Kikwete kutoka kwa Askofu Mkuu wa Kanisa la Wasabato Tanzania Ndugu Mark Warwa Marekana wakati wa Tamasha la la kuombea Amani kwenye Uchaguzi Mkuu ujao.
6
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akikata utepe ikiwa ni ishara ya uzinduzi rasmi wa album mpya ya Mwimbaji wa Nyimbo za Injili Ndugu Ben Mwaitege wakati wa Tamasha la kuombea Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu 2015 lililofanyika Uwanja wa Taifa hapa Dar es Salaam tarehe 4.10.2015.
8
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwahutubia maelfu ya wananchi waliohudhuria Tamasha la kuombea Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 lililofanyika kwenye Uwanja wa Taifa tarehe 4.10.2015.
10
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwapungia wananchi mbalimbali waliohudhuria Tamasha la kuombea Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu 2015 lililofanyika kwenye Uwanja wa Taifa tarehe 4.10.2015. PICHA NA JOHN LUKUWI.
1
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na Mchungaji Maboya mmoja wa viongozi walioshiriki Tamasha la kuombea amani kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
2
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa na maaskofu na wageni waalikwa wakifuatilia kwa makini waimbaji mbalimbali wa muziki wa injili kutoka Tanzania na nje ya nchi kwenye Tamasha la kuombea Amani kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 lililofanyika kwenye uwanja wa Taifa hapa Dar es Salaam tarehe 4.10.2015.
3
Mamia ya wananchi waliohudhuria Tamasha la kuombea amani kuelekea Uchaguzi mkuu wa Mwaka 2015 wakifuatilia wasanii mbalimbali wa nyimbo za injili waliokuwa wakiburudisha kwenye tamasha hilo lililofanyika kwenye uwanja wa Taifa tarehe 4.10.2015.
4
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwapungia wananchi waliohudhuria Tamasha la kuombea Amani kwa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kwenye Uwanja wa Taifa tarehe 4.10.2015. Anayepunga mkono kushoto ni Askofu Mkuu wa Kanisa la Wasabato Tanzania ndugu Mark Warwa Marekana.

No comments: