Wednesday, December 02, 2015

HUDUMA ISIYOKUWA NA USUMBUFU YA MAWASILIANO YAZINDULIWA

          Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Ian Ferrao akizungumza leo wakati wa uzinduzi wa huduma mpya inayojulikana kama Vodacom Red jijini Dar es Salaam leo.

 Ni  huduma ya Vodacom Red
 Inayotoa ofa nafuu na maalumu kwa wateja.

KAMPUNI ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania leo imezindua huduma mpya inayojulikana kama Vodacom Red ambayo imewalenga wateja wake wote wanaonunua muda wa maongezi kabla ya kupata huduma za mawasiliano ambayo ni bora zaidi,ina unafuu wa gharama na yenye kuwarahishia maisha.

Akiongea wakati wa uzinduzi jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania,Ian Ferrao amesema“Vodacom tumebuni huduma tukiwa tumewalenga wateja wetu wote hasa wale wenye shughuli nyingi ambao wanakosa  muda wa kununua vifurushi vya muda wa maongezi vya siku,wiki na vya mwezi.

Huduma ya Vodacom Red itawapatia unafuu wa kupiga simu kwa mitandao yote kwa gharama ya shilingi 1.5 kwa sekunde na kwa gharama hiyo hiyo ya shilingi 1.5 kwa sekunde watawezeshwa kupiga simu katika nchi tano kubwa zenye mtandao mkubwa wa masuala ya biashara ambazo ni (China,Afrika ya Kusini,India,Canada na Marekani),Kuhusiana na  matumizi ya data alisema wateja watakaotumia huduma hii watapatiwa kifurushi chenye unafuu kitakachowawezesha kupata huduma za intaneti yenye  kukidhi mahitaji yao”.

Kampeni hii inawarahisishia maisha watumiaji wake  kwa kutoa ofa  kwa watumiaji ambapo watafanya mawasiliano  kwa  kupiga simu  za ndani kwa malipo nafuu ya shilingi 1.5 kwa sekunde kwa mitandao yote pia kwa gharama hiyo hiyo ya shilingi 1.5 wanaweza kupiga simu kwenda nje ya nchi zipatazo 5 pia wanaunganishwa na huduma ya intaneti ya Mpango Mzima ambayo ina kasi kubwa na inawawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi  kwa muda wote.Katika kusherehekea uzinduzi wa huduma hii wateja watakaotumia shilingi 4,000/-na zaidi kwa kupiga simu za ndani watanufaika na mrejesho wa  asilimia 10% ya fedha hizo kupitia akaunti zao za M-Pesa kwenye simu zao.

Akiongelea mkakati wa Vodacom kuwaunganisha watanzania wote katika mtandao wa mawasiliano,Ferrao alisema “Lengo letu ni kuendelea kubuni huduma za kurahisisha mawasiliano kwa wateja wetu tukiwa na dhamira ya kuwapeleka katika ulimwengu wa sayansi na teknolojia.Vodacom Red ni mfano wa huduma ambayo imebuniwa  ikiwa ina ufanisi kubwa katika masuala ya biashara na yenye kuleta unafuu wakati huohuo kuwarahisishia maisha  wateja wetu”.

Wateja wa Vodacom wanaotumia huduma ya kuongeza salio kwenye simu zao kabla ya maongezi  wanaweza kuchangamkia huduma mpya na yenye unafuu mkubwa wa gharama.Ili mteja aweze kunifaika na huduma hii anachotakiwa kufanya ni kupiga *149*73# hapo mteja utapata frusa ya kuchagua anachokitaka kupitia huduma ya Vodacom Red.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na
Rosalynn Mworia
Head: Corporate Communications and PR
Mobile: +255754710661
Email: rmworia@vodacom.co.tz.

No comments: