Monday, November 30, 2015

WANASOKA WANAWAKE ZAIDI YA 400 WASHIRIKI TAMASHA LA LIVE YOUR GOALS

 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (katikati) akifuatilia kabumbu ya wanawake iliyokua ikiendelea wakati wa tamasha la Live Your Goals kuhamasisha mpira wa miguu wa wanawake lililoandaliwa na FIFA jana jijini Dar es Salaam katika viwanja vya Karume. Kulia ni Mkurugenzi wa Michezo Bw. Leonard Thadeo, na kushoto ni Mwenyekiti Kamati Soka la Vijana Bw. Ayoub Nyenzi.
 Baadhi ya wanasoka wanawake kutoka katika vilabu mbalimbali vya mpira wa miguu wakisakata kabumbu jana jijini Dar es Salaam katika viwanja vya Karume wakati wa tamasha la Live Your Goals kuhamasisha mpira wa miguu wa wanawake lililoandaliwa na FIFA.
  Mabalozi walioteuliwa na FIFA kuhamasisha mpira wa miguu wa wanawake nchini wakijitambulisha kwa mgeni rasmi wakati wa tamasha la Live Your Goals lilifanyika jana jijini Dar es Salaam katika Viwanja vya Karume kwa mara ya pili baada ya kufanya tamasha hilo kwa mara ya kwanza Mkoani Geita mnamo mwezi Julai 2015.
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (wapili kushoto) akimwangalia mtoto Zaynab Dotto mwenye umri wa miaka 10 anavyocheza na mpira kwa umahiri jana jijini Dar es Salaam katika Viwanja vya Karume. Kulia ni Mratibu wa Michezo ya Vijana wadogo Bw. Raymond Gweba na kushoto ni mama mzazi wa mtoto Zaynabu Bibi. Pili Said.

No comments: