Monday, November 16, 2015

BWANAUSI WA CCM ASHINDA UBUNGE JIMBO LA LULINDI

Aliyekuwa mgombea wa kiti cha ubunge katika jimbo la Lulindi kupitia CCM, Jerome Bwanausi ametangazwa kuwa mshindi wa kiti hicho baada ya kuwabwaga wenza watatu kutoka vyama vya NLD, CUF na ACT Wazalendo, katika uchaguzi mdogo uliofanyika jana.
Jerome ameshinda kiti hicho kwa kupata kura 17,715 sawa na asilimia 87.3, akifuatiwa na Modesta Makaidi wa chama cha NLD aliyepata kura 1,638, Amina Mshamu wa CUF akipata kura 714 na mgombea wa ACT Wazalendo Francis Ngaweje akiambulia kura 213.

No comments:

TUZINGATIE UTU, SHERIA NA HAKI KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YA ULINZI WA RASILIMALI ZA TAIFA- DKT KIJAJI

  Na. Joyce Ndunguru, Morogoro. Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Dkt Ashatu Kijaji (Mb) amewataka watumishi wa Mamlaka ya Usimamizi wa W...