Monday, November 16, 2015

BWANAUSI WA CCM ASHINDA UBUNGE JIMBO LA LULINDI

Aliyekuwa mgombea wa kiti cha ubunge katika jimbo la Lulindi kupitia CCM, Jerome Bwanausi ametangazwa kuwa mshindi wa kiti hicho baada ya kuwabwaga wenza watatu kutoka vyama vya NLD, CUF na ACT Wazalendo, katika uchaguzi mdogo uliofanyika jana.
Jerome ameshinda kiti hicho kwa kupata kura 17,715 sawa na asilimia 87.3, akifuatiwa na Modesta Makaidi wa chama cha NLD aliyepata kura 1,638, Amina Mshamu wa CUF akipata kura 714 na mgombea wa ACT Wazalendo Francis Ngaweje akiambulia kura 213.

No comments:

RAIS DKT.MWINYI AKAGUA MRADI WA MJI WA AFCON FUMBA, AANGALIA MAENDELEO YA UWANJA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Hussein Ali Mwinyi , leo Aprili 14, 2026, ameandika historia mpya baada ya kukagua ma...