Wednesday, November 25, 2015

MATUMIZI YA TEHAMA YABORESHA UFANISI SERIKALINI.


Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini toka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Florence Temba akiwaeleza waandishi wa habari (Hawapo pichani) kuhusu utaratibu wa Serikali kutumia TEHAMA katika kufanya mikutano kwa kutumia mfumo wa Mawasiliano ya (Video comference) ambapo kikao kimoja kitawaunganisha pamoja washiriki kutoka Mikoa 8 ambapo mada huwasilishwa na kutoa fursa ya kuwasiliana moja kwa moja (interactivity) kwa maswali na ufafanuzi leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari (MAELEZO) Bi Zamaradi Kawawa.
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bi Zamaradi Kawawa akifafanua jambo kwa waandishi wa Habari (hawapo pichani) wakati wa mkutano kati ya Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na vyombo vya habari uliofanyika leo jijini Dar es asalam.Kulia kwake ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini toka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Florence Temba na Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini toka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Priscus Kiwango.
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mkutano wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi kuhusu utaratibu wa Serikali kutumia TEHAMA katika kufanya mikutano ambapo mfumo wa Mawasiliano ya (Video comference) utatumika ili kupunguza gharama za mikutano kwa Taasisi za Serikali.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini toka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Florence Temba akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa Habari kuhusu faida za kutumia TEHAMA ikiwemo kuokoa fedha zilizokuwa zinatumika awali kuandaa mikutano hiyo ambapo kwa sasa washiriki watashiriki mikutano hiyo wakiwa katika vituo vyao vya kazi leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini toka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Priscus Kiwango. (Picha na Frank Mvungi-Maelezo)

No comments: