Tuesday, November 10, 2015

KAIMU MKURUGENZI MPYA AANZA KAZI, AKUTANA NA WATENDAJI MUHIMBILI

Aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Dk Hussein Kidanto (kushoto) akimtambulisha Kaimu Mkurugenzi mpya wa Hospitali hiyo, Profesa Lawrence Mseru (kulia) ambaye ameteuliwa jana na Rais John Pombe Magufuli. Jana Rais Magufuli amemuamishia Dk Kidanto katika Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.
MS2
Kaimu Mkurugenzi mpya wa Hospitali hiyo, Profesa Lawrence Mseru ambaye ameteuliwa jana na Rais John Pombe Magufuli akizungumza na menejimenti ya hospitali hiyo jana.
MS3
Baadhi ya wakurugenzi wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi mpya wa Hospitali hiyo Profesa Lawrence Mseru.
MS4
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma (MNH), Aminiel Aligaesha (kushoto) na mwanasheria wa hospitali hiyo, Veronica wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi mpya wa Hospitali hiyo Profesa Lawrence Mseru.
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
Kaimu  Mkurugenzi  Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence  Mseru leo ameanza kazi na kuwataka wafanyakazi wa hospitali hiyo kuwahi kazini kwa wakati na kufanya kazi kwa bidii.
Profesa Mseru ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es salaam  baada ya kukutana na menejimenti ya hospitali hiyo ambayo inajumuisha Wakurugenzi 14. Mkurugenzi huyo amekutana na menejimenti hiyo majira ya saa 6:00 mchana katika ukumbi wa mikutano wa hospitali hiyo.
Pia, amekutana na kamati tendaji ya hospitali , wakurugenzi, wakuu wa idara, mameneja wa majengo ikihusisha Sewahaji, Mwaisela, jengo la watoto na jengo la wazazi saa 8: 00 mchana.
Pamoja na mambo mengine katika kikao hicho, wakurugenzi  wameeleza mafanikio na changamoto mbalimbali zinazoikabili hospitali hiyo.
Profesa Mseru ameteuliwa jana kuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo baada ya Dk. Hussein Kidanto kuhamishiwa  wizara ya afya na ustawi wa jamii kwa ajili ya kupangiwa kazi nyingine.

No comments: