Tuesday, November 24, 2015

POP UP BONGO KUFANYIKA JUMAMOSI HII TRINITI OYSTERBAY DAR ES SALAAM

 
Nuya Essence
 
Founder of Branoz Collection Bahati Abraham with
customers
 
Secret Habits Seller servings customers
 
Pediah John, Founder of PSJ Brand with customers
copy
************************************************
Na Mwandishi Wetu
WASANII mbalimbali wa muziki na
maigizo pamoja na wadau wengine wa biashara watajumuika pamoja Triniti, Oyster
bay katika tamasha la biashara za bidhaa mbalimbali, Pop Up Bongo.
Tamasha hilo linalofanyika kila
baada ya miezi mitatu ni la siku moja na mwaka huu litafanyika tarehe 28 likiwa
chini ya udhamini wa kinywaji cha Smirnoff. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
Akizungumzia kuhusiana na tamasha
hilo mmoja kati ya waanzilishi wake, Natasha Stambuli alisema kuwa milango itafunguliwa
kuanzia saa mbili asubuhi na kuwa linatarajiwa kumalizika saa mbili usiku.
Alisema kuwa ikiwa ni kuelekea msimu
wa sikukuu za Christmas na mwaka mpya tamasha hilo linawakutanisha watu
mbalimbali na wamiliki wa maduka na wafanyabiashara za aina mbalimbali.
Alikuwa inakuwa ni nafasi nzuri kwa
watu mbalimbali pia kukutana na mbali na kufanyika kwa biashara kwenye eneo
hilo lakini pia inakuwa ni fursa ya kuburudika kwa kuwa kutakuwa na muziki na
vinwaji hivyo kuongeza furaha kwa watakaojitokeza.
“Ni mwishoni mwa mwaka
tunaelekea na kama mnavyojua kunakuwa na mambo mbalimbali wakati tukielekea
kufunga mwaka vijana wanataka kujua wapi pa kununua bidhaa mbalimbali kama nguo
na vinginevyo na Pop Up bongo inawapatia fursa hiyo hapo Novemba 27″ alisema
Natasha.
Aliongeza kuwa “kwa mwaka huu
wasanii pia wapo ambao watafika kuonana nao wadau wengine wa bidhaa
zinazowahusu kama nguo na nyinginezo na hakuna kiingilio kabisa.
Alisema kuwa wafanyabiashara ambao
kwa mwaka huu wataonesha bidhaa zao ni pamoja na Secret Habits, KAYA African
Collection, Nuya’s Essence, HIGHSUPDSM, FT boutique, Branoz Collections, ATSU,
Dress Kitenge, American Nails na wengineo wengi.

No comments: