Monday, November 30, 2015

MBUNGE WA JIMBO LA ILALA MUSSA ZUNGU ATEKELEZA AHADI ALIYOITOA WAKATI WA KAMPENI

  Mbunge wa Jimbo la Ilala Mussa Zungu (CCM) (mwenye kofia) akimkabidhi nahodha wa timu ya Ferry Beach Boys, Selemani Ally ‘Kaseja’ nyaraka za  Pikipiki  Dar es Salaam leo ambayo ilikuwa ni moja ya ahadi yake kwa kikosi hicho wakati wa kampeni.(PICHA NA  KHAMISI MUSSA)
 Mbunge wa Jimbo la Ilala Mussa Zungu (CCM) (mwenye kofia) akimkabidhi nahodha wa timu ya Ferry Beach Boys, Selemani Ally ‘Kaseja’ kibao cha namba za Pikipiki Dar es Salaam leo.   
 Zungu amesema  ilikuwa ni moja ya ahadi yake kwa kikosi hicho wakati wa kampeni alipofika kituoni hapo wakati alipopita kumuombea kura aliyekuwa mgombea  Urais Dk John Pombe Mgufuli  kupitia Chama cha Mapinduzi  CCM  ili iwasaidie kuongeza  kipato.
Mbunge huyo aliendelea kusema ataendelea kusaidia maswala ya michezo ili kuinua sekta hiyo kwa kusaidia vifaa  vya michezo Zungu ameongeza na kusema ” Leo nakusaidieni Pikipiki iwe mali ya timu si mali ya mtu,ya  wafanyabiashara wenyewe, na niliweka ahadi ya kuwawekea mahema kwenye maeneo mnayouzia samaki,  Nitatekeleza hilo  kabla ya mwezi wa kumi na mbili ili mfanye  biashara kwa uhuru.

No comments: