Monday, August 24, 2015

TANGA CEMENT YATOA SOMO LA UPANDAJI MITI KWA WANAFUNZI WA SEKONDARI YA ROSMINI

 Meneja Mawasiliano na Mahusiano ya Nje  wa Tanga Cement,Bi. Mtanga Noor (kulia) akiwa na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari  Rosmini ya mjini Tanga wakishiriki zoezi la kupanda miti katika hafla iliyoandaliwa na kampuni ya Saruji Tanga ikiwa na lengo la kutoa elimu kuhusu umuhimu wa kuhifadhi mazingira na elimu kwa vitendo kuhusu namna bora ya kupanda miti. Miti 316 ilipandwa katika hafla hiyo iliyofanyika Pongwe mkoani Tanga jana.
  Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari  Rosmini ya mjini Tanga wakimwagilia maji miti waliyoipanda katika hafla ya upandaji miti iliyoandaliwa na kampuni ya Saruji Tanga ikiwa na lengo la kutoa elimu kuhusu umuhimu wa kuhifadhi mazingira na elimu kwa vitendo kuhusu namna bora ya kupanda miti. Miti 316 ilipandwa katika hafla hiyo iliyofanyika Pongwe mkoani Tanga jana.
 Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari  Rosmini ya mjini Tanga wakishiriki zoezi la kupanda miti katika hafla ya upandaji miti iliyoandaliwa na kampuni ya Saruji Tanga ikiwa na lengo la kutoa elimu kuhusu umuhimu wa kuhifadhi mazingira na elimu kwa vitendo kuhusu namna bora ya kupanda miti. Miti 316 ilipandwa katika hafla hiyo iliyofanyika Pongwe mkoani Tanga jana.
 Meneja Usalama, Afya na Mazingira wa Tanga Cement, Leon Breed (kulia) akimsaidia mmoja wa wanafunzi wa shule hiyo, Douglas Mbarouk kupanda mti katika hafla hiyo.
Ofisa Usalama, Afya na Mazingira wa Tanga Cement, Augustine Mwanganga (kushoto) akiwaongoza baadhi ya wanafunzi hao katika zoezi la upandaji miti ambalo pamoja na kutoa elimu kwa mafunzo kuhusu upandaji miti lakini pia wanafunzi hao walifundishwa suala zima la umuhimu wa uhifadhi wa mazingira. 
 Mmoja wa wanafunzi wa Shule ya Rosmini High School, Clara Amon akimwagilia maji mti alioupanda katika hafla hiyo iliyofanyika katika eneo la Kiwanda cha Tanga Cement, Pongwe mjini Tanga jana. 

No comments: