Monday, August 31, 2015

WATEJA WA AIRTEL WAZAWADIWA MILIONI 25 KUPITIA PROMOSHENI YA JIONGEZE NA MSHIKO


Meneja Mauzo wa Airtel Kagera , Mohamed Kabeke (kushoto) akimkabithi
pesa taslimu  bwana Mwahamadi Katula (24) mfanyabiashara na mkazi wa
mkoa wa Kagera , mara baada ya kuibuka mshindi wa shilingi milioni 3
katika droo ya wiki ya tano ya promosheni ya Jiongeze na Mshiko
inayoendeshwa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel.
Afisa uhusiano na matukio, Dangio Kaniki akiongea na mshindi
aliyepatikana wakati wa kuchezesha droo ya sita ya wiki ya promosheni
ya "Jiongeze na Mshiko" ambapo wateja wawili wa Airtel kutoka mikoa ya
Mbeya na Dar es Salaam walipatikana akichukua taarifa za mshindi
(kushoto) ni mkaguzi kutoka bodi ya michezo ya kubahatisha bwana
Bakari Majid na Afisa huduma za ziada Airtel bwana Fabian
Felician.(kulia) droo hii imechezwa jana katika makao makuu ya Airtel
Moroco jijini Dar es saalam,.


KAMPUNI ya simu za mkononi ya Airtel imeendelea kuchezesha droo za
kila wiki na kuwazawadia  wateja wake jumla ya pesa taslimu shilingi
milioni 4 kila wiki baada ya kuibuka washindi katika droo za wiki za
promosheni hiyo.

Akizungumza wakati wa kuchezesha droo ya wiki ya sita ya promosheni hiyo
Meneja Uhusiano na Matukio wa Airtel Bi Dangio Kaniki alisema “ Tanga
tuanze promosheni hii mwenzi wa Julai mwaka huu tumeshuhudia wateja
wengi wakijishindia mamilioni ya fedha kila wiki na leo tumechezesha
droo ya wiki ya sita na kuweza kupata washindi wawili ambao nao
wamejishindia pesa taslimu akiwataja washindi hao Kaniki alisema” ninayo furaha kumtangaza Rajabu Mwanalipanga (19) Mwanafunzi na mkazi wa Dar es Salaam kuwa mshindi wa shilingi milioni 3 na mshindi wetu wa pili ni Bwana Frank Kapesa (22) mkulima na mkazi wa Mbeya amejishindia shilingi milioni 1 promosheni hii bado inaendelea tukiwa tumebakiwa na takribani wiki 10 za kuchezesha droo.  

Mpaka sasa shilingi milioni 25,000 zimeshatolewa
kwa washindi waliopatikana kutoka katika mikoa mbalimbali.  

Washindihao ni pamoja na John Luu na Josephat Mahinda wakazi wa Manyara, Mwahamadi Katula  Mkazi wa Kagera, Daudi Aliki na Agrisius Kapinga wakazi wa Dar es saalam, Rogers Shangali Mkazi wa Tanga, Gabriel
Ferdnandi  mkazi wa Musoma Mara, Hamisi Rashid mkazi wa Tabore, Rashid Hassani Mkazi wa Mtwara na Plasis Gabriel mkazi wa Geita.

Ili kushiriki mteja anatakiwa kutuma ujumbe wenye neno “BURE” kwenda
namba 15470, na kisha kuanza kupokea maswali kwenye simu zao na kujibu
maswali bure bila gharama yoyote na kujikusanyia pointi.

“ Jiongeze na Mshiko”  inamwezesha mteja kujiunga na kushiriki bure
kwa kujibu maswali na kujishinda shilingi milioni 1 kila wiki na
mwisho wa promosheni kujishindia milioni  2. 

 Na pia kumwezesha mteja
kujishindia zawadi kubwa zaidi  kwa kujiunga na ngazi ya Premium  kwa
kuchajiwa  shilingi 300 kwa siku na kupata nafasi ya kujishindia
shilingi milion 3 kila wiki na mwisho wa promosheni kujishindia

shilingi milioni 50.

No comments: