Monday, August 31, 2015

KANYAGA-TWENDE YA MAMA SAMIA YAMALIZIKA SINGIDA NA KUANZA DODOMA

Msafara wa Mgombea Mwenza wa Urais ka tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan, akitoka Singida mjini kwenda Dodoma, kupitia Ikungi na Manyoni kufanya mikutano ya kampeni leo.
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akimsalimia Mkuu wa wilaya mpya ya Ikungi, Gishuli Charles, alipowasili eneo la Makyungu, kufanya mkutano wa kampeni katika jimbo la Singida Kaskazini lililopo katika wilaya hiyo ya Ikungi. Kushoto ni Katibu wa CCM, Ikungi, Aluu Sagamba.
Wananchi wakimshangilia Mgombea mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan alipowasili eneo la Makyungu kuhutubia mkutano wa kampeni katika jimbo la Singida Kaskazini, wilayani Ikungi.
Wananchi wakiwa wamefurika kwenye mkutano huo wa Makyungu jimbo la Singida Kaskazini
Mkuu wa mkoa wa Singida Parseko Kone akimsalimia Mkuu wa wilaya mpya ya Ikungi.
 Kada wa CCM aliyeko katika kampeni za Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM akionyesha furaha kutokana na mambo kwenda vizuri katika mkutano wa kampeni wa Makyungu,jimbo la Singida Kaskazini. Continue reading

No comments: