Saturday, August 22, 2015

SUMAYE AITOSA CCM, AJIUNGA UKAWA


Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye akiongea na wanahabari.
Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye, leo  amekihama Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kujiunga na Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA).
Sumaye amejiunga rasmi na Ukawa wakati wa mkutano wa wanahabari na viongozi wa Umoja huo,  mkutano uliofanyika mchana wa leo katika ukumbi wa hoteli ya Kunduchi jijini Dar.
Aidha Sumaye hakusema ni chama gani amejiunga nacho, licha ya kubainisha lengo lake kuu la kuondoka CCM ni kwenda kuimarisha Ukawa na kuongeza nguvu kwenye vyama vya upinzani hasa katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25.

No comments:

WAZIRI NA NAIBU WAZIRI WA ARDHI WASHIRIKI KIKAO CHA KWANZA CHA MKUTANO WA 19 WA BUNGE LA 12 KWA AJILI YA KUJADILI BAJETI YA SERIKALI 2025/2026

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Deogratius Ndejembi (MB), leo tarehe 8 Aprili 2025, ameshiriki kikao cha kwanza cha Mku...