Thursday, August 20, 2015

INNOCENT MELLECK SHIRIMA ACHUKUA FOMU ZA UBUNGE JIMBO LA VUNJO


Mgombea wa nafasi ya Ubunge katika jimbo la Vunjo,Innocent Shirima akitia saini katika kitabu cha wageni mara baada ya kufika ofisi za msimamizi wa Uchaguzi katika jimbo hilo ambaye ni mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Moshi.

Mgombea Ubunge jimbo la Vunjo ,Innocent Shirima akikabidhiwa fomu za kuwania ubunge katika jimbo la hilo na msiamizi wa Uchaguzi ,Fulgence Mponji ambaye pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo.
Mgombea Ubunge wa jimbo la Vunjo kupitia chama cha Mapinduzi, Innocent Shirima akionesha fomu zake za kuwania Ubunge katika jimbo hilo.
Mgombea Ubunge katika jimbo la Vunjo, Innocent Shrima akiwa na makada waliomsindikiza wakatialipofika ofisi za msimamizi wa uchaguzi kwa ajili ya kuchukua fomu.Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Knada ya Kaskazini.

No comments: