Sunday, July 26, 2015

RAIS KIKWETE AMUAPISHA MKURUGENZI MPYA WA UCHAGUZI BW. KAILIMA RAMADHANI KOMBEY JIONI HII IKULU


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akimuapisha Ndugu Kailima Ramadhani Kombwey kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi Ikulu jijini Dar es salaam Julai 25, 2015.
Ndugu Kailima Ramadhani Kombwey akiweka sahihi kwenye hati baada ya kuapishwa kuwa kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi Ikulu jijini Dar es salaam  Julai 25, 2015.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akiweka sahihi baada ya muapisha Ndugu Kailima Ramadhani Kombwey kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi Ikulu jijini Dar es salaam Julai 25, 2015.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akikabidhi vitendea kazi baada ya kumuapisha Ndugu Kailima Ramadhani Kombwey kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi Ikulu jijini Dar es salaam Julai 25, 2015.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mikono na Ndugu Kailima Ramadhani Kombwey baada ya kumuapisha kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi Ikulu jijini Dar es salaam jioni ya leo Julai 25, 2015.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Ndugu Kailima Ramadhani Kombwey kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi Ikulu jijini Dar es salaam Julai 25, 2015. Wengine kutoka kushoto ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Florens Turuka, Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Hamid Mohamoud Hamid, Rais Kikwete, Ndugu Kailima Ramadhani Kombwey, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue na Msajili wa vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi.
Rais Kikwete akiwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi mpya Ndugu Kailima Ramadhani Kombwey
 
Rais Kikwete akisalimiana na mtoto wa Ndugu Kailima Ramadhani Kombwey, Msemakweli (2) wakati wa hafla hiyo fupi.
 PICHA NA IKULU

No comments: