Friday, July 24, 2015

MABALOZI INDIA,UBELGIJI NA SWEDEN WAMUAGA RAIS KIKWETE IKULU

1
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na balozi wa India anayemaliza muda wake Mhe.Debnath Shaw wakati balozi huyo alipokwenda kumuaga ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo ameagana na mabalozi watatu wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania baada ya kumaliza muda wao wa kazi .
Mabalozi walioagana na Rais leo ikulu jijini Dar es Salaam ni pamoja na Mhe.Debnath Shaw wa India,Balozi Koenraad Adam  wa Ubelgiji na balozi Lennarth Hjelmaker wa Sweden.
2
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na balozi Koenraad Adam wa Ubelgiji ikulu jijini Dar es Salaam alipokwenda kumuaga.
4
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na balozi wa Sweden nchini aliyemaliza muda wake Mhe.Lennarth Hjelmaker ikulu jijini Dar es Salaam 
3
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Balozi wa Sweden nchini aliyemaliza muda wake Mhe.Lennarth Hjelmaker ikulu jijini Dar es Salaam 
(picha na Freddy Maro)

No comments: