Friday, July 24, 2015

MAMA SALMA AWASILI MALAYSIA NA KUTEMBELEA KIWANDA CHA KUTENGENEZA TRENI CHA SMH RAIL MJINI KUALA LUMPUR


 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokea ua kutoka kwa watoto wa wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Malaysia mara baada ya kuwasili kwenye Hoteli ya Royale Chulan iliyopo Kuala Lumpur, Mji Mkuu wa Malaysia tarehe 23.7.2015.
 Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA, Mama Salma Kikwete akipokewa na Mkurugenzi Mkuu wa SMH Rails Bwana Narayanan Kuppusamy mara baada ya kuwasili kwenye karakana ya treni iliyoko Kuala Lumpur nchini Malaysia Tarehe 24.7.2015.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokea ua kutoka kwa Mke wa Mkurugenzi Mkuu wa SMH Rails Mama Lakshmi Narayanan ikiwa ni ishara ya kumkaribisha kutembelea karakana ya treni na mabehewa huko Malaysia tarehe 24.7.2015.


No comments: