Sunday, July 19, 2015

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AHITIMISHA BARAZA LA SIKUKUU YA EID EL- FITRI KITAIFA MKOANI GEITA.

1
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia katika Barala la Sikukuu ya Eid El- Fitri iliyofanyika Kitaifa kwenye Ukumbi wa Shule ya Sekondari Wasichana ya Nyankumbu, mkoani Geita Julai 18, 2015.
Picha na OMR
4
Baadhi ya Waumini wa dini ya Kiislamu waliohudhuria Baraza la Sikukuu ya Eid El- Fitri, wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Geita, Bi Fatma Maswi, wakimsikiliza Makamu wa Rais, Dkt. Bilal, wakati akihutubia katika Baraza hilo lililofanyika Kitaifa Mkoani Geita Julai 18, 2015.
5
Kaimu Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir Ally, akizungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi Makamu wa Rais Dkt. Bilal, kuhutubia katika Baraza hilo.
6
Katibu Mkuu wa Baraza la Waislamu Tanzania, (BAKWATA) Suleiman Lolila, akizungumza, kabla ya kumkaribisha Kaimu Mufti.
7
Mkuu wa Mkoa wa Geita, Bi Fatma Maswi, akizungumza kuwakaribisha wageni katika hafla hiyo ya Baraza la Sikukuu ya Eid El- Fitri.
8
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Sheikh  Haruna Abdallah Kichwabuta, akitoa neno la shukrani baada ya hafla hiyo na Makamu wa Rais Dkt. Bilal kuhutubia.

No comments:

WAZIRI MKUU MHE. KASSIM MAJALIWA AMALIZA ZIARA YA SIKU MOJA MKOANI MBEYA

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), leo ameondoka Mkoani Mbeya baada ya kukamilisha zi...