Saturday, July 18, 2015

MUSTAFA PANJU ACHUKUA NA KURUDISHA FOMU YA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA ARUSHA MJINI AAHIDI UMOJA NA MAENDELEO

SAM_3880
Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Bushbucks Safaris iliyopo jijini Arusha Mustafa Panju ambaye ni mmoja wa wagombea wa jimbo la Arusha mjini kupitia chama cha mapinduzi CCM akimkabidhi Katibu wa CCM wilaya ya Arusha, Ferooz Bano fomu ya kuwania kinyang’anyiro hicho baada ya kuchukua fomu hiyo jana na kurejesha huku akisisitiza kuwa endapo atafanikiwa kupitishwa na chama hicho au laa atashirikiana na wananchi pamoja na wanaCCM katika kuleta maendeleo katika jimbo hilo ambalo lipo mikononi mwa chama cha Demokrasia na maendeleo( CHADEMA).
Habari Picha na Pamela Mollel wa jamiiblog)
SAM_3827
Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Bushbucks Safaris iliyopo jijini Arusha Mustafa Panju ambaye ni mmoja wa wagombea wa jimbo la Arusha mjini kupitia chama cha mapinduzi CCM akionyesha fomu ya kuwania nafasi ya ubunge baada ya kukabidhiwa na Katibu wa CCM wilaya ya Arusha, Ferooz Bano jana katika ofisi za CCM wilaya
SAM_3886
Hapa Mustafa Panju akiandika jina lake katika fomu yenye majina ya waliokuja kuchukua fomu kupitia chama hicho kwa  Katibu wa CCM wilaya ya Arusha, Ferooz Bano ,kushoto ni mke wake aliyemsindikiza kuchukua fomu
SAM_3889
Katibu wa CCM wilaya ya Arusha, Ferooz Bano akionyesha kadi ya mgombea ubunge kupitia chama cha CCM Mustafa Panju

No comments: