Tuesday, July 21, 2015

KAMANDA WA POLISI MKOA WA PWANI JAFARI IBRAHIMU AZUNGUMZIA JUU YA SILAHA ZILIZOKAMATWA

ki1
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishina mwandamizi Jafari Ibrahimu akifafanua jambo kwa waandishi wa habari ofisini kwake kuhusina na watuumiwa wa ujamabzi waliokamatwa pamoja na siraha ambazo wamezikamata baada ya kufanya operesheni katika mapori(Picha na Victor Masangu)
ki2
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishina mwandamizi Jafari Ibrahimu akifafanua jambo kwa waandishi wa habari ofisini kwake kuhusina na watuumiwa wa ujamabzi waliokamatwa pamoja na siraha ambazo wamezikamata baada ya kufanya operesheni katika mapori(Picha na Victor Masangu)
………………………………………………….
VICTOR MASANGU, PWANI
 
KUFUATIA kukithiri kwa wimbi la matukio ya uharifu pamoja na kuvamia vituo vya polisi  Jeshi la polisi Mkoa wa Pwani  limefanya msako mkali katika mapori mbali mbali  na  kufanikiwa kuwanasa watuhumiwa  wa ujambazi  27 pamoja na   risasi 153,bunduki 2  mabomu 3  ambavyo  walikuwa wakivitumia katika matukio ya uharifu.
 
Akizungumza na wa waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishina mwandamizi Jafari Ibrahimu amesema kwamba watuhumiwa hao wamekamatwa baada ya kufanyika operesheni katika magenge yaliyopo vichakani na kuwakuta watuhumiwa hao wakiwa wamejificha.
 
 Kamanda amesema kwamba  wameamua kufanya  operesheni  hiyo  kutokana na kuongezeka kwa uharifu katika baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Pwani na kuwakamata watuhumiwa hao  ambao wengine walikutwa na vifaa mbali mbali ikiwemo visu mapanga,pamoja na nyaya tatu za milipuko ya mabomu.
 
Aidha Kamanda huyo amebainisha kwamba katika zoezi hilo pia waliweza  kukamata madawa ya kulevya aina aya bangi gunia 18 na mirungi kilo 124,lita 88 za pombe ya moshi pamoja na mitambo yake mitatu ya kutengenezea noti bandia 370 na meno ya tembo.
 
 Katika hatua nyingine Kamanda huyo amesema kwamba wanafunzi wawili  wa familia moja katika shule ya msingi mgogodo  iliyopo Wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani wamepoteza maisha  baada ya chumba chao walichokuwa wamelala kuteketea kwa moto na kwamba chanzo cha moto huo ni kibatali.
 
 Mkoa wa pwani umekuwa na matukio ya uharifu mbali mbali ikiwemo kuvamiwa kwa vituo vya polisi ikiwemo kituo cha  Kimazichana Wilayani mkuranga ,Ikiwiriri ,kituo kidogo cha mloka,pamoja na tukio la kufanya  jaribio la kutaka kuvamia kituo cha polisi Kibiti vyote vilivyopo Wilayani Rufiji.

No comments: