Tuesday, March 03, 2015

WAZIRI WA UJENZI DKT MAGUFULI AHITIMISHA ZIARA YAKE WILAYA YA SAME NA MWANGA MKOANI KILIMANJARO.

 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli katikati akiweka jiwe na msingi kuashiria kuanza kwa ujenzi wa barabara ya Mwanga-Kikweni-Vuchama-Usangi-Lomwe yenye urefu wa kilomita 40. Kulia kwake ni Waziri wa Maji ambaye pia ni Mbunge wa Mwanga Profesa Jumanne Maghembe, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama pamoja na viongozi wengine wa Wilaya ya Mwanga.
 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli kushoto akizungumza jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Musa Iyombe kabla ya kuweka jiwe la msingi katika barabara ya Mwanga-Kikweni-Vuchama-Usangi-Lomwe yenye urefu wa kilomita 40.6. Katikati ni Waziri wa Maji ambaye pia ni Mbunge wa Mwanga Profesa Jumanne Maghembe.
 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama wakicheza ngoma na kikundi cha ngoma za asili Kikweni kabla ya uzinduzi wa barabara ya Mwanga-Kikweni-Vuchama-Usangi-Lomwe yenye urefu wa kilomita 40.
 . Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli akipiga ngoma na kikundi cha ngoma cha Msanja group kabla ya kuhutubia mamia ya wakazi wa Usangi kuhusu ujenzi wa barabara ya Kikweni-Usangi-Lomwe ambayo itaanza kujengwa hivi karibuni.
 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli kushoto akizungumza jambo na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mama Ana Kilango Malecela katika sehemu ya Kihurio.Dkt. Magufuli ametangaza kujengwa kilomita tatu za lami katika eneo hilo pamoja na kuifanyia maandalizi ya kujengwa kwa kiwango cha lami barabara ya Mkomazi-Same yenye urefu wa km 96.
 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiwahutubia mamia ya wakazi wa Kihurio Same Mkoani Kilimanjaro.
 Wakazi wa Usangi waliojitokeza kumsikiliza Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli
 Waziri wa Ujenzi akiwahutubia wakazi wa Gonja wakati akipita kukagua barabara ya Kihurio hadi Gonja maore Wilayani Same Mkoani Kilimanjaro.

 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiagana na wananchi wa Usangi mara baada ya kuwahutubia.
Picha ya Pamoja Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli katikati akiwa pamoja na Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama, pamoja na Viongozi wengine wa Wilaya na Chama cha Mapinduzi mara baada ya kuhitimisha ziara yake katika Wilaya za Same na Mwanga mkoani Kilimanjaro.Picha zote kwa Hisani ya Kitengo cha Mawasiliano-Wizara ya Ujenzi

No comments: