Wednesday, March 25, 2015

KINANA, CYRIL CHAMI, LEONIDAS GAMA WAVUNA MPUNGA

1Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kazi ya kuvuna Mpunga na Mbunge wa jimbo la Moshi Vijijini Dr. Cyril Chami na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mh. Leonidas Gama wakati katibu mkuu huyo alipotembelea mashamba ya umwagiliaji ya Mabogini Moshi Vijijini, ambapo amekagua miradi mbalimbali ya maendeleo na kushiriki katika kazi mbalimbali za mikono pamoja na wananchi, Kinana yuko katika ziara ya kikazi mkoani Kilimanjaro akikagua, kuhimiza  na kusimamia utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM akiongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi. (PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-MOSHI VIJIJINI-KILIMANJARO)2Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na viongozi wenzake wakiendelea na kazi ya kuvuna mpunga.003Mpunga ukiwa umestawi katika mashamba hayo.3Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na Mkuu wa wilaya ya Moshi mjini Ndugu Novatus Makunga kulia wakati walipowasili katika kata ya Mabogini.4Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wananchi mbalimbali wa kata ya Mabogini.5Mbunge wa jimbo la Moshi Vijijini Mh. Dr. Cyril Chami akizungumza na wananchi wa kata ya Mabogini.6Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akwahutubia wananchi katika kata ya Mabogini Moshi Vijijini wakati alipowatembelea.7Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisaini kitabu cha wageni huku akizungumza na Mkuu wa Chuo cha Ufundi cha Kibosho Maadam Anna na kulia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro Ndugu Iddi Juma.8Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  akizungumza na wanafunzi wa Chuo cha Ufundi cha Kibosho na walimu pamoja na wananchi wakati alipotembelea chuo hicho ambacho kimejengwa kwa nguvu za wananchi na marafiki wa Kibosho Education Trust Fund pamoja na Mbunge wa jimbo hilo Mh. Dr. Cyril Chami.9Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipanda mti katika chuo cha ufundi cha Kibosho.10Wasanii wakiimba wimbo kumkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati alipowasili katika kata ya Kibosho Kati kwa ajili ya mkutano wa hadhara.11Wasanii wakiimba wimbo kumkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati alipowasili katika kata ya Kibosho Kati kwa ajili ya mkutano wa hadhara.

No comments: