Monday, March 30, 2015

MHE. WILLIAM LUKUVI AKIZUNGUMZA NA WADAU KUHUSU MPANGO WA UENDELEZAJI WA MJI MPYA WA KIGAMBONI

3
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Willium Lukuvi akisisitiza jambo wakati wa mkutano na wadau kuhusu mpango wa uendelezaji wa mji mpya wa Kigamboni, Dar es Salaam. Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Bw. Meck Sadiki. Sehemu ya wadau hao ni pamoja na viongozi wa taasisi za Serikali, mashirika yasiyo ya Kiserikali (NGO’s), madhehebu mbalimbali ya dini na taasisi za elimu na ulinzi na huduma mbalimbali zilizopo katika eneo hilo la Kigamboni.
2
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angellah Kairuki akizungumza katika mkutano na wadau kuhusu mpango wa uendelezaji wa mji mpya wa Kigamboni, Dar es Salaam.
4
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk. Sellasie Mayunga akizungumza jambo wakati wa mkutano huo.
6
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Bibi Sophia Mjema akizungumza wakati wa mkutano huo.
5
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Willium Lukuvi pamoja na Naibu wake Mhe. Angellah Kairuki wakimsikiliza mmoja wa wadau Bw. Nyaronyo Kicheere nje ya ukumbi wa mkutano.