Tuesday, March 31, 2015

KINANA AMALIZA ZIARA YAKE ROMBO, AVUNA WANACHADEMA TARAKEA

1Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki katika kazi ya kutandaza nyaya za umeme vijijini pamoja na wafanyakazi wa TANESCO wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro katika kijiji cha Kirongo Samanga wakati akiwa katika ziara yake katika jimbo la Rombo akikagua na kuhimiza ilani ya Uchaguzi ya CCM mwaka 2010  ya inayotekelezwa na serikali huku akihimiza uhai wa chama cha mapinduzi. Katika ziara hiyo Kinana anaongozana na katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Taifa CCM Ndugu Nape Nnauye.(PICHA NA KIKOZIKAZI CHA FULLSHANGWE-ROMBO-KILIMANJARO)2Mafundi wa TANESCO wakiendelea na kazi ya kusa baza umeme katika kijiji cha Kirongo Samanga wilayani Rombo.018Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Bw. Shanel Ngowi Mkurugenzi wa kiwanda cha kutengeneza Juisi na Maji cha Bella View kilichopo katika Bella.019Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipiga picha na wafanyakazi wa kiwanda cha Juice Bella View.017Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kiwanda cha  juisi cha Bella View Bw. Shanel Ngowi alipokagua uzalishaji wa kiwanda hicho.020Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoa heshima zake katika kaburi la pamoja la wanafunzi wa shule ya sekondari ya Shauritanga waliofariki katika ajali ya moto miaka kadhaa iliyopita mkoani Kilimanjaro. 3Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo ya mradi wa maji wa Kahe kutoka kwa Mhandisi wa maji wilaya ya Rombo Bw.Tesha Andrew wakati alikagua mradi huo.4Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na baadhi ya wananchi wakati alipokagua mradi wa maji wa Kahe wilayani Rombo.5Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiunganisha maji wakati alipokagua ujenzi wa  mradi wa maji wa Kahe wilaya ya Rombo.6Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akifungua maji ya bomba wakati alipokagua ujenzi wa mradi wa maji katika kijiji cha Kahe wilayani Rombo.7Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na injinia wa maji wilaya ya Rombo Bw. Tesha Andrew.8Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wananchi mbalimbali wakati alipowasili katika uwanja wa Polisi Tarakea wilayani Rombo ambapo mkutano wa hadhara umefanyika.9Baadhi ya wananchi wakiwa katika mkutano huo10Wananchi wa Tarakea wakinyanyua mikono yao juu  wakati mkutano huo ukiendelea.111213Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia maelfu ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa polisi mjini Tarakea.1415Mmoja wa akina mama wa CCM akiwasili kwa pikipiki katika eneo la mkutano mjini Tarakea wilayani Rombo.16Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Bw. John Saimon aliyekuwa Katibu wa CHADEMA wilaya ya Rombo na Katibu wa Mbunge wa jimbo hilo Mh. Joseph Selasini akitangaza rasmi kujiunga na CCM katika mkutano wa hadhara mjini Tarakea.17Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikusanya kadi za vijana wa CHADEMA waliojiunga na CCM katika mkutano huo.18Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimvisha kofia Bw. John Saimon  mara baada ya kujiunga na CCM.19Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana aki na Kijana John Saimon wakipigiana saluti mara baada ya kumalizika kwa mkuta no wa hadhara katikati anayeshuhudia ni Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Taifa.

No comments: