Tuesday, March 24, 2015

KINANA: TUTAHAKIKISHA TUNAIRUDISHA CCM YA WAKULIMA NA WAFANYAKAZI YENYE KUWATETEA WANYONGE

Kinana amewaasa wana CCM kukemea vitendo vibaya vya viongozi wa serikali na watendaji wanaokiuka utaratibu wa kazi na kufanya mambo yasiyokuwa ya kimaadili katika utendaji wao. Ili kukiweka chama hicho katika sura nzuri kwa wananchi, “Wana CCM tunatakiwa kuwa wa kwanza kukemea maovu siyo  wana CCM tunaanza kuwalinda na kuwatetea waovu jambo ambalo si sawa kabisa,  Tutahakikisha tunairudisha CCM ya wanyonge na masikini watoto wa wakulima na wafanyakazi aliyoiacha Baba wa Taifa Mwalimu J.K.Nyerere”,  Katika ziara hiyo Kinana anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-HAI-KILIMANJARO)
6Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akizungumza na wana CCM wa wilaya ya Hai mara baada ya mapokezi ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.5Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na viongozi wa mkoa wa Kilimanjari wakishiriki kuchimba msingi wa jengo la darasa wakati aliposhiriki ujenzi wa madarasa katika  shule ya msingi Modio Masama Mashariki wilayani Hai.3Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akijulia hali Mzee Israel Elly Nawinga aliyewahi kuwa Waziri wa Elimu na Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa miaka ya nyuma nyumbani kwake Masama Mashariki, wa kwanza Kulia ni Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mh. Leonidas Gama na katikati ni Mkuu wilaya ya Hai Ndugu Anthony Mtaka.2Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akijulia hali Mzee Israel Elly Nawinga aliyewahi kuwa Waziri wa Elimu na Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa miaka ya nyuma nyumbani kwake Masama Mashariki, Kulia ni Mkuu wa wilaya ya Hai Ndugu Anthony Mtaka.4Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mh. Leonidas Gama akimsalimia  Mzee Israel Elly Nawinga aliyewahi kuwa Waziri wa Elimu na Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa miaka ya nyuma nyumbani kwake Masama Mashariki, wakati Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alipomtembelea nyumbani kwake Masama Mashariki wilaya i Hai.9Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua daraja la Mnepo kijiji cha Kiyungi wilayani Hai lililojengwa na serikali.8Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kupaka rangi katika kingo za  daraja la Mnepo kijiji cha Kiyungi wilayani Hai lililojengwa na serikali wakati alipokagua ujenzi wa daraja hilo.7.Daraja la Mnepo katika kijiji cha Kiyungi likiwa katika hatua mbalimbali za ujenzi10Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akivuka katika daraja la awali lililokuwa likitumiwa na wananchi ambapo wananchi hao wamesema watu wengi wamepoteza maisha na kuumia wakati wakivuka daraja hilo kwa kipindi chote ambacho kulikuwa hakuna daraja imara na la kudumu.
11Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akivuka katika daraja hilo.13Baadhi ya wajumbe wa mkutano mkuu wa wilaya ya Hai wakiwa katika mkutano mjini Boma Ng’ombe.14Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza katika kutano wa wajumbe wa mkutano mkuu wa wilaya ya Hai.15Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na wananchi wa kijiji cha Mtakuja ambacho wakazi wake na majirani zao wana mgogoro mkubwa wa mipaka ya ardhi na kiwanja cha ndege cha KIA mkoani Kilimanjaro.16Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwapungia mkono wananchi hao mara baada ya kuwasili kijijini hapo.17Wananchi hao wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana. 18Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mtakuja wilayani Hai.19Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumzana wauguzi na madaktari wakati alipotembelea katika hospitali ya wilaya ya hai mkoani Kilimanjaro.20Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizunguma na wauguzi na madaktari wa hospitali hiyo.21Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua baadhi ya mashine katika chumba cha miozni hospitalini hapo.22Nape Nnauye akifanyiwa vipimo katika chumba cha mionzi hospitalini hapo.23Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipiga picha ya pamoja na madaktari na wauguzi pamoja na watumishi wengine wa hospitali hiyo.24Nape Nnauye akihutubia katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Snow View Boma Ng’ombe wilayani Hai.25Mamia ya wananchi wakiwa katika mkutano huo.26Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara kwenye viwanja vya Snow View Boma Ng’ombe wilayani Hai.27Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisisitiza jambo wakati akihutubia katika mkutano huo.28Kikundi cha vijana kikiimba wimbo maalum katika mkutano huo.29Madereva wetu kutoka kulia ni Mick Mzee wa Cremia, Prosper na Adam Soud.

No comments: