Monday, February 04, 2013

WAFANYAKAZI WA SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA (NHC) WAKARIBISHA MWAKA KWA SHANGWE




Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akiserebuka na mkewe kwenye sherehe hiyo, hoteli ya Serena juzi Jumamosi.
******************

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu amesema kwamba kipaumbele cha Shirika hilo kwa sasa ni kujenga nyumba za gharama nafuu nchi nzima ili mkuwawezesha Watanzania wengi zaidi kuwa na makazi bora na yenye staha kwa maisha yao.
Akizungumza kwenye sherehe za kuuga mwaka 2012 na kuukaribisha mwaka 2013, alisema kwamba mwelekeo wa sasa wa shirika ni kuwekeza nguvu zote katika kuhakikisha makazi bora nay a bei nafuu yanapatikana kwaajili ya wananchi wa Tanzania.
“Lengo letu kwa mwaka huu ulioanza majuzi ni kuhakikisha tunajenga nyumba nyingi zaidi za gharama nafuu nchi nzima ili kuwezesha watanzania wengi zaidi kumiliki makazi bora na kuwaondolea adha ya kuyakosa makazi hayo,”alisema.
Alisema Shirika lake katika utekelezaji wa mpango mkakati wa Shirika unaolenga kujenga nyumba 15,000 hadi kufika mwaka 2015 , Shirika hilo litahakikisha linaweka mikoani majengo ya heshima ambayo yatakuwa kioo kwa majengo mengine yote na hivyo kuboresha uchumi wa mikoa husika lakini pia kupendezesha mikoa hiyo.
“Tumeazimia angalau kila mkoa tulipo tunajenga iconic building ambalo litapendezesha mji , lakini pia litainua hali ya uchumi ya mikoa husika kwa kuwa tukishajenga majengo yenye hadhi na usalama wa uhakika , basi taasisi na asai mbalimbali za kiuchumi zitanunua au kupanga katika majengo yetu na kwa kufanya hivyo uchumi wa maeneo husika utapanda,”alisema.
Katika shughuli hiyo, Mchechu aliwaomba wafanyakazi kuendelea kujituma pamoja na kukabiliana na ushindani wa kikazi sambamba na kuhakikisha wanafanikiwa kuendesha maisha yao kwa kutumia vyanzo mbalimbali vya kujipatia kipato.
Alisema hivi sasa Shirika limejiwekea mfumo wa kutathimini utendaji ambapo wale ambao wataonekana kuwa wamefanya kazi bora zaidi watazawadiwa na wale ambao wanaonekana kulega lega watakumbushwa na wanaoshindwa kabisa hatakuwa na budi kuagana nao ili kusudi kuwatendea haki wanayostahili kwa kazi wanayofanya.

 Dk naye Kabogo naye hakuwa mbali kusakata ngoma ya Baikoko
 Wafanyakazi wakisakata rhumba
 Wanaingia ukumbini
 Utamu wa ngoma

 Hawa vijana wanapatikana pale
  Mkurugenzi Mkuu, Nehemia Mchechu akimlisha keki mke wa mfanyakazi aliyefanya kazi muda mrefu zaidi Shirikani, Bwana Mwakigosi (kushoto). Mwakigosi amefanya kazi NHC tangu mwaka 1979.
 Mwenyekiti wa TAMICO, Daniel Nkya akigongesha glasi na wafanyakazi wenzake
 Mkurugenzi Mkuu, Nehemia Mchechu
 MC wetu Ephraim Kibonde akifanya mambo yake
 Mdau Itandula Gambalagi (mwenye shati jeupe) akibadilishana mawazo na Veronica Mtemi (aliyesimama)
Mke wa Mkurugenzi Mkuu akicheza na baadhi ya wafanyakazi wake hapa ilikuwa ni katika miondoko ya kwaito.

No comments: