Wednesday, February 27, 2013

Spika Makinda akutana na Balozi wa Jamhuri ya Namibia nchini Tanzania Balozi Japhet Issack

 Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Anne S. Makinda (kushot)  akimkaribisha Balozi wa Jamhuri ya Namibia nchini Tanzania Balozi Japhet Issack alipomtembelea ofisini kwake leo.Pamoja na mambo mengine Balozi huyo amemuomba Spika Makinda kuimarisha uhusiano  na Bunge la Namibia kwani kuna mambo mengi Bunge hilo linaweza kujifunza kutoka Tanzania.
  Spika Makinda akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na Balozi wa Namibia nchini Tanzania ambapo amemhakikishia Balozi huyo kuwa Bunge la Tanzania lipo tayari kushirikiana na Bunge la Namibia na kuona ni maeneo yapi ambayo yatawafaidisha wananchi wa  nchi mbili hizi. Aliainisha maeneo ya mafunzo na kujenga uwezo kuwa ya kipaumbele.Picha Na Prosper Minja-Bunge.

No comments:

MHE. NDEJEMBI AHIMIZA USHIRIKIANO WA WAKUU WA MIKOA NA WILAYA KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA NISHATI

Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, leo tarehe 22 Januari, 2026, amezungumza katika Mkutano wa Tathmini ya Utekelezaji wa Mkataba w...