Tuesday, February 05, 2013

Rais Jakaya Kikwete na Mama Salma Kikwete Watembelea Ujenzi wa Daraja la Mto Malagarasi wilayani Uvinza mkoani Kigoma.




 Picha Zote na IKULU
--
 Rais Jakaya Kikwete jana amefanya ziara ya siku moja mkoani Kigoma na kukagua maendeleo ya Ujenzi wa daraja la Kikwete katika Mto Malagarasi wilayani Uvinza mkoani Kigoma.


Rais Kikwete alitembelea daraja hilo na kuzungumza na wananchi wa eneo jirani na daraja hilo na kuwataka walitumie vyemka katika kuwaletea maendeleo ikiwa ni pamoja na kutumia ardhi yao kwa kilimo na si kuiuza kwa watu wengine.

Kikwete amewaambia wakazi hao kuwa wasikubali kulubuniwa na wageni wanaokuja kama wawekezaji na kununua maelfu ya hekta za ardhi yao.

No comments:

NHC YAKABIDHI MSAADA KWA WATU WENYE ULEMAVU UBUNGO

  Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kupitia kwa Afisa wake Mkuu wa Habari, Yahya Charahani, limekabidhi msaada wa vifaa vya kusaidia watu we...