Thursday, February 14, 2013

IPYANA AONDOKA NA HYUNDAI YA ECO BANK

  Mkurugenzi Mkuu wa Ecobank, Enoch Osei-Safo akizungumza wakati wa kutoa zawadi kwa mshindi wa shindano la shinda na Babkubwa.
  Ipyana Mwakasaka akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukabidhiwa zawadi yake.
 
Mkuu wa Ecobank, Enoch Osei-Safo (kushoto) akimkabidhi funguo ya gari aina Hyundai Tucson ix35 lenye thamani ya shilingi milioni 65 mshindi wa shindano la Shinda na Babkubwa.

 Mkuu wa  Kitengo cha Sekta ya Umma wa Ecobank, Ndabu Swire akizungumza wakati wa hafala ya kutoa zawadi kwa mshindi wa Shindano la Babkubwa lililoendeshwa na benki hiyo jijini Dar es Salaam leo.
 Ipyana Mwakasaka akijaribu kifaa chake alichokabidhiwa mchana huu na Ecobank baada ya kuibuka mshindi katika shindano la Shinda na Babkubwa lililoendeshwa na benki hiyo.
******
MKAZI wa Tegeta Dar es Salaam, Ipyana Mwakasaka, ameibuka mshindi wa zawadi ya gari aina ya Hyundai Tucson ix35 lenye thamani ya shilingi milioni 65, katika shindano la Shinda na Babkubwa, lililokuwa likiendeshwa na Benki ya Ecobank ya jijini Dar es Salaam.

Mshindi huyo alitangazwa jana jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi na Wafanyabiashara Wadogo wa Ecobank, Joyce Malai, kuhitimisha shidano la miezi sita na kusimamiwa na Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini.

Malai alisema kuwa, shindano hilo lilianza rasmi Juni mwaka jana na kudumu hadi Desemba, huku washindi wa zawadi za kompyuta mpakato ‘laptops’, vocha za manunuzi na tiketi za ndege wakipatikana, kabla ya mchakato wa kumpata mshindi wa zawadi kuu.

“Walengwa walikuwa ni wateja binafsi, wajasiriamali, kampuni ndogondogo na za kati (SMEs), likiwa na dhumuni la kutanua uelewa wa Watanzania juu huduma za Ecobank, ikiwamo kuimarisha tamaduni chanya ya watu kujiwekea akiba katika taasisi za kifedha,” alisema Malai.

Malai aliongeza kuwa, Ecobank imejipanga kuendelea kuwaboreshea huduma wateja wake kwa mwaka huu wa 2013, sambamba na mageuzi mengine chanya yanayofanywa na benki inayotoa huduma katika mataifa 33 barani Afrika.

Akizungumza baada ya kupokea funguo za gari aina hiyo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Ecobank, Enoch Osei-Safo, Mwakasaka aliishukuru benki hiyo kwa kuwajali wateja na kutimiza ahadi ya kukabidhi zawadi hiyo ambayo hakuitarajia, ingawa imekuja wakati muafaka.

“Nimefurahi kuwa mshindi na kupata zawadi ya gari la thamani kubwa ambalo sikuwa na ndoto ya kulimiliki. Naishukuru Ecobank, huku nikiwataka Watanzania kutumia huduma za benki hii na kuepuka utunzaji pesa majumbani ambao ni hatari,” alisema Mwakasaka.

1 comment:

Anonymous said...

I am sure by the end of it facilitator; I testament offer creative
slipway to get the duet moving in a new management. comfortably now, if you're thought process correct you use Christian marriage counseling, tierce areas testament be given care by the attendance counsellor. almost marriages scramble through some rocky marriage is in hassle and then it is.

my web blog :: marriage counseling las vegas