Friday, February 08, 2013

LICHA YA KUSHIKA MOTO: MV VICTORIA YAELEKEA BUKOBA KAMA KAWA


Mv Victoria ikijitayarisha kwa ajiri ya kufanya safari yake usiku wa leo kuelekea mjini Bukoba mkoani Kagera mara baada ya kukaguliwa kufuatia kunusurika kuteketea mchana wa leo kupitia sakata la wachomeleaji walio sababisha moto uliozuka eneo la kuhifadhi mizigo.

Mv. Victoria ikipakia gari usiku huu hatimaye kuanza safari yake usiku huu.

Nao wasafiri walipanda kama ada licha ya baadhi yao kuonekana kuwa na wasiwasi na wengine kuahirisha kabisa safari.

Ndani ya meli abiria wakitathimini mazingira.

Saa 3 na dakika 10 meli ya Mv. Victoria iliondoka Mwanza.... kuelekea Bukoba mkoani Kagera.
Picha na Mdau G sengo wa Clouds FM

No comments: