Monday, August 18, 2014

WAREMBO WA MISS TANZANIA KUVAA NGUO ZA S &D COLLECTION

DSC_0307
Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania Bw. Hashim Lundenga akimtambulisha Mkurugenzi wa Kampuni ya S&D Collection iliyotangaza udhamini wa shindano la Miss Tanzania Bi. Devotha Kajogoo Mtambo kulia wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye hotli ya JB Belmonte jijini Dar es salaam.
DSC_0341
Mkurugenzi wa Kampuni ya S&D Collection Bi. Devotha Kajogoo Mtambo akisisitiza wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye hotli ya JB Belmonte jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania Bw. Hashim Lundenga na kulia ni Bi.Esther Maro Mkurugemzi wa S&D Collection 
…………………………………………………………….
Na Majuto Omary
Kampuni ya S &D collection kwa upande wa Boutique imetangaza udhamini wa nguo kwa warembo wote 30 watakao wania taji la Miss Tanzania 2014  watakaopambana mwezi  Oktoba jijini.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jumatatu, mkurugenzi wa S&D Collection, Devota Kijogoo Mtambo alisema kuwa hatua ya kudhamini mashindano hayo ni kujihusisha katika shughuli za kijamii mbali ya kujitangaza kupitia jukwaa hilo.
Devota alisema kuwa warembo wote 30 watazawadiwa nguo kuanzia shoo ya ufunguzi, vazi la  ubunifu, ufukweni na warembo watano watakaoingia katika hatua ya fainali. Alisema kuwa pia watadhamini nguo za mshindi wa taji la Miss Tanzania ambaye ataiwakilisha nchi katika mashindano ya mwakani ya kumsaka mrembo wa dunia.
“Lengo letu ni kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Kampuni ya Lino International Agency ya kuendeleza mashindano ya urembo hapa nchini, ni mashindano makubwa na ndiyo maana sisi tumeingia kutokana na ubora wake na ubora wa bidhaa zetu,” alisema Devota.
Alisema kuwa kampuni yao itatumia si chini Dola za Kimarekani 27,000 (zaidi ya Sh Milioni 44) kwa ajili ya nguo za warembo hao.
Mkurugenzi wa Lino International Agency, Hashim Lundenga aliipongeza kampuni hiyo kwa kudhamini mashindano hayo na wameikubali kutokana na uwekezaji wake katika shughuli hiyo.
“Mashindano yetu ni makubwa, kampuni ya S&D Collection ni kubwa na imewekeza vilivyo katika mashindano yetu, hii itasaidia kuongeza ubora huku warembo wakipata hafueni kwani hawataingia katika gharama za mavazi,” alisema Lundenga.
Alisema kuwa kwa sasa wanaendelea na mashindano ya Kanda kabla ya kuanza maandalizi ya kambi ya Taifa mara baada ya kukamilika kupatikana kwa warembo wote 30.

No comments: