Friday, August 29, 2014

JOPO LA MAJAJI LA KUMTAFUTA MSHINDI WA TUZO YA RAIS YA HUDUMA ZA JAMII NA UWEZESHAJI YAENDELEA NA ZOEZI LAKE JIJINI TANGA NA WILAYA YA MKINGA

Picha Na 1
Majaji  Bw.  Venance Bahati (kushoto) na Bi.  Costansia Gabusa (kulia) wakijadiliana jambo wakati wa kufanya tathmini ya  mradi wa ukingo uliojengwa pembezoni mwa bahari kwa ajili ya kuzuia mmomonyoko katika eneo la  Mwarongo jijini Tanga. Ukingo huo umejengwa kwa msaada wa kampuni ya utafutaji wa mafuta na gesi ya Afren PLC.
Picha Na 2Mwalimu Mkuu  wa Shule ya Sekondari ya Tongoni Bw.  Mzihili Abeid (kushoto) akitoa maelezo mbele ya majaji waliotembelea maabara ya shule hiyo. Maabara hiyo  imejengwa na  kampuni ya utafutaji wa mafuta na gesi ya Afren PLC.
Picha Na 3Msimamizi wa kampuni ya  utafutaji  wa mafuta na gesi  ya Afren PLC Bw. Ahmed Omar (kulia) akizungumza  na jopo la majaji na sektretarieti  kwenye maabara ya shule ya sekondari ya  Tongoni  iliyofadhiliwa na kampuni  hiyo.
Picha Na 4Jaji  Venance Bahati (katikati) akiteta jambo na msimamizi wa kampuni ya utafutaji  wa mafuta na gesi ya Afren PLC Bw. Ahmed  Omar (kulia). Kushoto ni Jaji Costansia Gabusa.
Picha Na 5Msimamizi wa kampuni ya  utafutaji  wa mafuta na gesi  ya Afren PLC Bw. Ahmed Omar (kushoto) akizungumza na majaji  walipotembelea maabara ya Shule ya Sekondari ya Mabokweni  jijini Tanga ambapo kwa sasa kampuni hiyo imejitolea kuwajengea maabara  ya kisasa.
Picha Na 6Mkurugenzi wa kampuni ya  Dawson Food Products Ltd iliyopo wilayani Mkinga mkoani Tanga Bw. Burhani Taibali (kulia) akizungumza na majaji pamoja na sekretarieti iliyotembelea  kampuni hiyo.

No comments: