Wednesday, August 27, 2014

TIMU YA MAJAJI KWA AJILI YA KUMTAFUTA MSHINDI WA TUZO YA RAIS YA HUDUMA ZA JAMII NA UWEZESHAJI YAANZA KAZI RASMI WILAYANI HANDENI MKOANI TANGA

 Jaji Venance Bahati ( kulia) na Jaji Constancia Gabusa (kushoto) wakijadiliana jinsi ya kuanza zoezi la kumtafuta mshindi wa  Tuzo ya Rais ya Huduma za Jamii na Uwezeshaji   nje ya  Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Handeni mara baada ya  timu hiyo kuwasili katika wilaya ya Handeni kwa ajili ya zoezi hilo. Zoezi  hili linahusisha makampuni yanayojishughulisha na shughuli za madini, gesi na mafuta ambapo mshindi katika utoaji  wa huduma bora kwa  jamii na uwezeshaji atakabidhiwa tuzo yake mapema Novemba, mwaka huu.
 Afisa Mipango wa  Halmashauri ya Handeni Bw.  Dawson Temu akielezea jinsi makampuni ya utafutaji madini  yanavyochangia katika huduma za jamii katika wilaya ya Handeni mbele ya timu ya majaji (hawapo pichani) ofisini kwake.
 Jaji Constancia Gabusa (kushoto) na  Kaimu Afisa Madini Mkazi  wa Handeni Bw. Jared Obado (kulia) wakifuatilia kwa makini maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Afisa Utawala wa Wilaya ya Handeni Upendo Magashi (hayupo pichani)
 Jaji Venance Bahati (kushoto) akikagua moja ya  ofisi za waalimu katika shule ya msingi ya Nyasa zilizojengwa na kampuni ya  utafutaji wa madini ya Canaco katika zoezi la kutathmini miradi  iliyofadhiliwa na kampuni hiyo
 Mmoja wa wakazi wa kijiji cha Nyasa ( wa pili kutoka kulia) ambaye  jina lake halikupatikana mara moja akielezea mchango wa makampuni ya  utafutaji wa madini katika huduma  za jamii ndani ya kijiji  hicho.
 Mkuu wa Mradi wa  Kampuni ya Utafutaji wa Madini ya  Canaco Bw.  John Holana (kulia) akielezea mchango wa kampuni hiyo katika uendelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika kijiji cha Nyasa ikiwa ni pamoja na maji, shule na mkakati wa kujenga kituo cha afya. Kushoto ni mmoja wa majaji Bi. Constancia Gabusa.
 Mkuu wa Mradi wa  Kampuni ya  Utafutaji wa Madini ya  Canaco Bw.  John Holana akitoa maelezo mbele ya majaji pamoja na wajumbe wengine wa kijiji cha Nyasa mafanikio yaliyopatikana tangu kuanzishwa kwa kampuni hiyo.
 Mjiolojia Mkuu kutoka  Kampuni ya  Utafutaji wa Madini ya Douglas Lake Minerals Bw.  Godfrey Bitesigirwe akielezea changamoto wanazokumbana nazo  katika utoaji  wa  huduma bora kwa  jamii inayoizunguka kampuni hiyo mbele ya majaji waliotembelea kampuni hiyo (hawapo pichani) kwa ajili ya kuendelea na zoezi la kumtafuta mshindi  wa Tuzo ya Rais ya Huduma za Jamii na Uwezeshaji.
 Jaji Constancia Gabusa akitoa  ushauri kwa kampuni  ya Utafutaji wa Madini ya Douglas Lake Minerals jinsi  ya kukabiliana na changamoto  katika utoaji wa huduma bora kwa jamii inayowazunguka ikiwa ni pamoja na umuhimu wa kuwashirikisha wananchi katika mipango  ya miradi ya maendeleo
Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi ya Nyasa Bw.  Ali Mhada akielezea  mchango wa kampuni  ya utafutaji wa madini  ya Canaco katika kutoa ufadhili kwa wanafunzi waliofanya  vizuri kama mkakati mmojawapo wa kuwajengea wanafunzi uwezo wa kuwa wataalamu wa baadaye na kufanya kazi katika kampuni hiyo.

No comments: